Mtoto wa miaka minane amekutwa akiwa amepakiwa katika
begi la nguo na kusafirishwa kinyemela kwenye mpaka wa Hispania na eneo la
Afrika Kaskazini, polisi wa nchi hiyo wamesema.
Mtoto huyo aitwaye Abou kutoka Ivory Coast alegunduliwa
baada ya polisi wa Ceuta, jirani na Morocco, kuweka begi hilo kwenye mashine ya
kupimia na kugundua kivuli cha kitu kisichokuwa cha kawaida.
Baada ya kulifungua walimku walimkuta mtoto, akiwa
katika hali mbaya.
Hali ya wasiwasi aliyokuwa nayo mbebaji wa begi hilo,
mwanamke mwenye umri wa miaka 19 raia wa Morocco, iliwafanya polisi kumtilia
shaka katika kivuko cha El Tarajal na hivyo kupelekea kulipima begi hilo kwenye
mashine maalumu. Alikamatwa na saa
kadhaa baadaye baba wa mtoto huyo, raia wa Ivory Coast akakamatwa kwenye mpaka
huo.
Kwa mujibu wa gazeti la Hispania la El Pais, mwanamke
aliyebeba begi hilo alilipwa pesa na baba wa mtoto huyo ili kumfanyia kazi
hiyo.
Baba wa mtoto huyo, ambaye pia anaitwa Abou, ameripotiwa
kuishi katika visiwa vya Canary nchini Hispania na alitarajia mwanaye huyo
aungane naye.
Kila mwaka, maelfu ya wahamiaji na wanaotafuta hifadhi,
ambao wanakimbia matatizo mbalimbali katika nchi zao, hujaribu kuvuka kuptokea
Morocco kwenye Hispania kupitia kwenye mlango bahari wenye ukubwa wa kilometa
15 wa Gibraltar.
Wahamiaji hao hutumia mitumbwi na boti zisizokuwa na
usalama na kuifanya safari yao kuwa ngumu na ya mashaka.
Kadhalika, maelfu ya wahamiaji hujaribu kuingia Hispania
kupitia miji ya Ceuta na Melilla karibu na mpaka wa nchi hiyo na Morocco. Serikali
ya Hispania imeweka uzio wenye urefu wa mita saba ili kuwazuia wahamiaji wasiingie
katika eneo la nchi hiyo.
Wahamiaji wengine hujaribu kuvuka mpaka kwa kujificha
ndani ya magari ya mizigo, kuogelea au kuvuka kwa majahazi kwenye pwani ya
Morocco na kuingia Hispania.
0 comments:
Post a Comment