CROATIA WAPIGA KURA KUPINGA NDOA ZA JINSIA MOJA

 Croatians voted overwhelmingly in support of a ban on same-sex marriage on December 1, 2013. (File photo)


Wananchi wa Croatia wamepiga kura kwa wingi katika kura ya maoni ya kupiga marufuku ndoa za jinsia moja, hatua inayonekana kuwa ni pigo kwa serikali iliyokuwa ipiga kampeni dhidi ya mabadiliko hayo.

Matokeo rasmi ya awali yanaonesha kuwa asilimia 65.76 wanataka katiba itamke wazi kuwa ndoa ni “muungano baina ya mwanaume na mwanamke.”

Matokeo hayo yatakapothibitishwa yatawekwa katika katiba na hivyo kuzipiga marufuku ndoa za jinsia moja.

Aidha, matokeo hayo ni pigo kwa Waziri Mkuu Zoran Milanovic na Rais Ivo Josipovic, ambao waliwataka wananchi kupiga kura ya “hapana” kukataa mabadiliko hayo.

Baada ya Waziri Mkuu kupiga kura yake, alisema kuwa kura hiyo ya ya maoni ni yenye kuhuzunisha na isiyokuwa na maana.

Bunge la nchi hiyo lililazimika kuitisha kura ya maoni baada ya zaidi ya wananchi  740,000 kusaini waraka unaotaka kuitishwa kwa kura hiyo ya maoni.

Kampeni hiyo ilianzishwa na kundi moja la wananchi na kuungwa mkono na chama cha upinzani cha Croatian Democratic Union.

Kundi hilo lilitaka tafsiri ya ndoa iwekwe katika katiba ili kwamba watu watakapotaka kufanya mabadiliko watahitaji zaidi ya theluthi mbili ya kura za wabunge.


Hata hivyo, serikali ya nchi hiyo imesema kuwa wiki chache zijazo itapeleka bungeni muswada wa sheria utakaowapa haki zaidi wanandoa wa jinsia moja.

Baada ya ukamilishaji wa mchakato huo, Croatia itaungana na kundi la nchi za Ulaya kama vile, Poland, Belarus, Moldova, Bulgaria, Montenegro na Serbia, ambazo zimepiga marufuku ndoa za jinsia moja katika katiba zao.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment