WAHANGA 71 WA MAUAJI YA KIMBARI YA SREBRENICA WAZIKWA HUKO BOSNIA NA HERZEGOVINA

 IHA Photo

Hatimaye mabaki ya miili ya wahanga 71 wa mauaji ya Srebrenica yamezikwa leo ikiwa ni kumbukumbu ya 22 ya mauaji makubwa kabisa ya kimbari yaliyotokea barani Ulaya tangu mauaji ya Holocaust.

Mnamo Julai 11 mwaka 1995 zaidi ya Wabosnia 8,000, wengi wao wanaume na vijana, waliuawa kinyama na wanajeshi wa Serbia kwa amri ya Jenerali Ratko Mladić.

Zaidi ya watu 20,000 walikusanyika kuomboleza mauaji hayo huku ndugu na wanafamilia waliokuwa kwenye eneo la kumbukumbu la mauji hayo nchini Bosnia wakibubujikwa na machozi kwa kuwapoteza ndugu na jamaa.

Baada ya swala ya adhuhuri, miili ya wahanga hao ambayo ilitambuliwa mwaka jana baada ya kupatikana kwa makaburi ya pamoja katika misitu na viwanda, ilizikwa katika eneo la makaburi la Potoçari.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, alitoa salamu zake za rambirambi kwa wanafamilia wa wahanga hao, na kuelezea namna walinda amani wa Umoja huo walivyoshindwa katika jukumu lao walipopelekwa huko.

Alisisitiza kuwa jumuiya ya kimataifa, na hasa Umoja wa Mataifa, inabeba jukumu kwa masaibu hayo ya Srebrenista. Pia aliashiria kuwa Umoja huo umekuwa ukiyafanya kazi mapungufu hayo na kujifunza kutokana na makosa yaliyopita.


"Tunatakiwa kuyatazama kwa dhati yaliyopita, kutambua uhalifu uliotokea na ubaridi uliosababisha yakatokea na kuhakikisha kwamba mauaji kama hayo hayajirudii tena," alisema Guterres.


Mwaka 2007 mahakama ya Kimataifa ya Haki iliyatambua mauaji hayo ya Srebrenica kuwa ni mauaji ya kimbari.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment