MUBARAK NA WANAYE WAHUKUMIWA MIAKA 3 JELA

 Egypt’s deposed dictator, Hosni Mubarak, waves from his room at the Maadi military hospital in Cairo on May 4, 2015. © AFP

Mahakama nchini Misri imetoa hukumu ya kifungo cha miaka mitatu jela kwa rais wa zamani wa nchi hiyo, Husni Mubarak, na wanaye wawili kwa makosa ya ufisadi.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka nchini humo, mahakama hiyo imemtia hatiani Mubarak na wanaye wawili, Alaa na Gamal, kwa makosa ya ubadhirifu wa fedha ya umma zilizokuwa zimetengwa kwa ajili ya ukarabati wa ikulu ya Rais.

Mahakama imetoa adhabu ya kifungo cha miaka mitatu kwa kila mmoja, na kuwaamuru kulipa faini ya kiasi cha dola milioni 16.4, ambazo ndio kiasi cha pesa zilizoibiwa.


Haijawa wazi iwapo uamuzi huo wa mahakama utaangalia muda ambao watatu hao wameshautumia gerezani.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment