WAKIMBIZI 5 WAUAWA, WENGINE WAJERUHIWA NCHINI RWANDA


 


Kwa uchache wakimbizi watano wameuawa na wengine 20 kujeruhiwa kwenye kambi moja nchini Rwanda baada ya maandamano ya kupinga hatua ya upunguzaji wa chakula kutawaliwa na ghasia, jeshi la polisi nchini humo limesema. Polisi saba pia walijeruhiwa.

Wakimbizi wapatao 3,000 waliweka kambi nje ya ofisi za Umoja wa Mataifa kwenye kambi hiyo tangu Jumanne. Siku ya Alhamisi polisi walijaribu kuwatawanya kwa kutumia mabomu ya kutoa machozi, msemaji wa polisi Theos Badege ameiambia redio ya serikali.

“Tulitumia nguvu jana mchana baada ya kutoa onyo kwamba vikosi vya usalama vitatumika,” alisema.

“Walianza kurusha mawe na vyuma, na hapo wakimbizi 20 na maafisa saba wa polisi wakajeruhiwa. Wakimbizi watano walifariki dunia.”

Wakimbizi kumi na tano walikamatwa, jeshi la polisi limesema kupitia mtandao wa Twitter.

Wakimbizi hao kutoka nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo waliondoka kambini katika eneo la Kiziba na kutembea kwa miguu umbali wa kilometa 15 (maili 10) mpaka Karongi, magharibi mwa Rwanda, kupinga hatua ya Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) kukata asilimia 25 ya mgao wa chakula mwezi uliopita. Kambi hiyo inawahifadhi wakimbizi 17,000 kutoka Kongo.


Rwanda imewahifadhi wakimbizi wapatao 174,000, wakiwemo wakimbizi 57,000 kutoka nchi jirani ya Burundi ambao walikimbia ghasia nchini mwao mwaka 2015. Wengine waliobaki waliikimbia Kongo kwa sababu za ukosefu wa uthabiti nchini mwao zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Mnamo mwezi Januari, UNHCR ilisema kuwa ingepunguza mgao wa chakula kutokana na uhaba wa ufadhili wa huduma zake.

Mapema Alhamisi shirika hilo lilisema ilipokea asilimia 2 tu ya ufadhili kwa mwaka 2018 kwa ajili ya huduma zake nchini Rwanda ambao ni dola milioni 98.8, huku Shirika la Chakula Duniani likionya kuwa litapunguza zaidi chakula iwapo mahitaji yake ya kila mwezi ya dola milioni $2.5 hayatotekelezwa.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment