DUTERTE: WAPIGENI RISASI WAASI WANAWAKE SEHEMU ZA SIRI


Duterte's spokesman said the president's jokes are 'funny' and that critics should lighten up [Jeoffrey Maitem/Getty Images]
Rais wa Ufilipino, Rodrigo Duterte




Rais wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, amekosolewa vikali na mashirika ya haki za binadamu baada ya kusema kuwa waasi wa kike wa kundi la kikomunisti nchini humo wanatakiwa kupigwa risasi katika sehemu zao za siri kama adhabu yao kwa kufanya uasi dhidi ya serikali.


Tangazo la Duterte ni sehemu ya mfululizo wa kauli zenye utata alizozitoa kuhusu wanawake, shirika la haki za binadamu la Human Rights Watch limesema katika tamko lake.


"Ni kauli inayowahamasisha askari wa serikali kufanya dhulma za kijinsia katika uwanja wa mapambano, jambo ambalo ni ukiukaji wa sheria ya kimataifa ya haki za binadamu," amesema mwakilishi wa Human Rights Watch nchini humo bwana Carlos Conde.


Kwa mujibu wa hotuba iliyotolewa Februari 7, bwana Duterte alisema kuwa askari wa serikali wanatakiwa kuwapiga risasi waasi wa kike sehemu zao za siri.


"Tutawapiga risasi kwenye sehemu zenu za siri, ili kwamba ukikosa sehemu za siri, msiwe na faida yoyote," alisema Duterte katika lugha ya kikabila ya Visayan, ambayo huzungumzwa katika eneo la kati na kusini mwa Ufilipino.


Aidha, rais huyo aliwalaumu vikali wanawake hao waasi kwa kuwatekeleza watoto na familia zao na kwenda kujiunga na kikundi hicho cha waasi wa kikomunisti.


Emmi de Jesus, mbunge kutoka chama cha Wanawake cha Gabriela Women's Party, alilaani vikali kauli tata ya Duterte na kusema kuwa itachangia kueneza utamaduni wa uvunjaji wa sheria nchini humo.


MSEMAJI: DUTERTE ANAPENDA SANA UTANI


Duterte amekosolewa mara kadhaa kwa kauli zake zenye utata dhidi ya wanawake.


Mwezi Januari, wakati wa ziara yake nchini India, aliwaambia wafanyabiashara wakubwa wa India na Ufilipino mjini New Delhi kuwa angependa kuwavutiwa wawekezaji kuwekeza katika nchi yake kwa kuwapa ofa ya wanawake bikra 42.


Mnamo Julai 2017, alifanya utani wa vitendo vya ubakaji kuhusu Miss Universe.


Miezi miwili kabla, Duterte aliwaambia askari waliokuwa wakipigana na wapiganaji wa Kiislamu katika eneo la Marawi kuwa wakitaka wanaweza kubaka wanawake watatu na hawatoadhibiwa.


"Nitawafunga jela mimi mwenyewe," alisema, akitoa tahadhari kwa askari wanaokiuka sheria. Kisha akasema: “Lakini ukibaka wanawake watatu, nitakubali, sitakuwa na shida nalo hilo.”


Wakati wa kampeni zake za urais mwaka 2016, wakosoaji wake walikasirishwa sana alipoelezea tukio la ghasia za gereza moja lililotokea mwaka 1989 ambapo Mmisionari mmoja wa Kiaustralia aliuawa, na wafungwa walipanga msitari kwa ajili ya kumbaka.


Duterte alisema kuwa mwanamama huyo alikuwa “mrembo” na yeye kaka meya wa mji wa Davao lilikotokea tukio hilo, alitamani kuwa wa kwanza kupanga foleni kumbaka mwanamke huyo. Baadaye aliomba radhi na kusema kuwa hakukusudia kuvunja heshima ya wanawake au waathirika wa ubakaji.


Mapema Jumatano, msemaji wa Duterte, Harry Roque, alitetea kauli tata za rais huyo akisema kuwa wakosoaji wake wanapaswa kuwa waelewa.


"Unajua, wakati mwingine, watetezi hawa wa mambo ya wanawake wanakuwa na mhemko sana”, alisema Roque.


"Ninamaanisha kuwa huo ni mzaha tu. Msikuze mambo. Furahini basi,” alisema msemaji huyo wa Duterte.


Utawa wa Duterte umekuwa ukifanya mazungumzo ya mara kwa mara ya kusaka amani na waasi hao wa kikomunisti tangu alipoingia madarakani katikati mwa mwaka 2016.



Lakini kufuatia kuibuka kwa mapambano mapya kati ya vikosi vya serikali na waasi hao mwaka 2017, Duterte alisaini tangazo lililowaorodhesha waasi hao kama kundi la kigaidi, na hivyo kukatisha mchakato wa kusaka amani.


Pia aliagiza kutiwa nguvuni kwa viongozi kadhaa wa kikomunisti.


Chama hicho cha Kikomunisti kilianza uasi nchini humo kwa 1968 ambapo mpaka sasa zaidi ya watu 30,000 wamepoteza maisha.


Kundi la uasi la New People's Army limekuwa likipambana na serikali ya Ufilipino tangu mwaka 1968


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment