KAGAME MWENYEKITI MPYA WA UMOJA WA AFRIKA

 


Rais wa Rwanda, Paul Kagame amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Umoja wa Afrika katika mkutano wa kilele cha umoja huo unaofanyika katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa.

Bwana Kagame anapokea kijiti hicho cha uongozi kutoka kwa Rais wa Guinea, Alpha Conde. Ataongoza umoja huo kwa muhula wa mwaka mmoja.

Katika hotuba yake ya kukubali uteuzi huo, Kagame alizitaka nchi za Afrika kuungana, kuunda soko la pamoja la Afrika, kuunganisha miundombinu na kushirikisha uchumi na teknolojia.

Ili kufanikisha malengo yake, Kagame aliwataka viongozi wa Afrika kumuunga mkono.

“Ahsanteni kwa imani yenu kubwa. Kwanza kama kiongozi wa mchakati wa mabadiliko na sasa kama mwenyekiti wa umoja wetu.” Kagame alisema. “Ninaahidi kufanya kazi bora. Lakini ninahitaji mniunge mkono kikamilifu.”

Kagame anatumai kuona umoja huo ukijitegemea na kuacha kuwa tegemezi baada ya uamuzi uliofanywa kwamba nchi zote wanachana zitenge asilimia 0.2 ya kodi ya bidhaa kutoka nje kufadhili shughuli za umoja huo.



Afrika “inakaribia” kuwa na eneo huru la biashara”, alisema mwenyekiti huyo mpya. “Ukweli hilo linatakiwa kufanyika mwaka huu.”
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment