AFGHANISTAN: WATU WENYE SILAHA WASHAMBULIA CHUO CHA JESHI MJINI KABUL

Security officials closed off roads leading to the Marshal Faheem Military academy, after an attack in Kabul [Jawad Jalali/EPA]
Maafisa wamezifunga barabara zinazoelekea katika Chuo cha kijeshi cha Jemedari Faheem baada ya shambulizi lililotokea leo mjini Kabul.



Chuo kimoja cha jeshi katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, kimeshambuliwa na kusababisha askari wawili kupoteza maisha, siku chache baada ya zaidi ya watu 100 kuuawa katika mlipuko jirani na jengo la wizara ya mambo ya ndani.

Msemaji wa ikulu ya nchi hiyo amesema kuwa washambuliaji hao hawakuweza kuingia ndani ya Chuo Kikuu cha Ulinzi wa Taifa cha Jemedari Fahim – ambalo ni shambulio kubwa la tatu katika mji huo ndani ya wiki mbili.

Shambulizi hilo limedaiwa kufanywa na kundi la wapiganaji wa Dola la Kiislamu katika Iraq na Sham (ISIL) kupitia tovuti ya kundi hilo ya Amaq.

Aidha, mbali na askari hao wawili, kwa uchache askari 10 wamejeruhiwa, huku washambuliaji wanne wakiuawa na mmoja kukamatwa.

Mashambulizi yanaendelea katika kikosi cha polisi jirani na chuo hicho, maafisa wamesema.

Shambulizi la leo limetokea wakati wakazi wa mji huo wakiwa na maumivu kutokana na shambulizi la kujitoa mhanga lililotokea siku ya Jumamosi katika eneo la katikati ya mji, ambalo liliua zaidi ya watu 100 na wengine 91 kujeruhiwa.


Mji wa Kabul tayari ulikuwa kwenye tahadhari kubwa, huku ulinzi ukiimarishwa hasa jirani na eneo la mlipuko huo – eneo la karibu na jengo la wizara ya mambo ya ndani, hospitali ya Jamhuriat, ofisi za serikali, maeneo ya biashara na shule.

Kundi la Taliban lilidai kuhusika na shambulizi la Jumamosi, likisema kuwa liliwalenga maafisa wa serikali.

Abdullah Fahimi, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Abu Rayhan mjini Kabul, aliliambia shirika la habari la Al Jazeera kuwa mji huo umeshuhudia ongezeko kubwa la mashambulizi yanayofanywa na makundi ya waasi katika misimu miwili ya majira ya baridi iliyopita.

"Haya yanatokea kutokana na mkakati mkali uliofanywa na serikali ya Afghanistan na serikali ya Marekani, ambazo ziliwawekea vikwazo wanachama sita wa kundi la Taliban Mtandao wa Haqqani," Fahimi amesema.

Taarifa zaidi itawajia...


CHANZO: Aljazeera




Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment