DUTERTE AAMURU WAFANYAKAZI WA KIFILIPINO KUONDOKA KUWAIT NDANI YA SAA 72

Philippine President Rodrigo Duterte shows a photo of a Filipina worker in Kuwait, of whom he said she had been roasted like a pig, during a press conference in Davao City, in the southern island of Mindanao on February 9, 2018. (AFP Photo)
Rais wa Ufilipino Rodrigo Duterte akionesha picha ya mfanyakazi wa Kifilipino aliyekuwa akifanya kazi nchini Kuwaita, ambaye anasema kuwa alichomwa kama nguruwe, wakati wa mkutano na waandishi wa habari katika mji wa Davao, katika kisiwa cha kusini mwa nchi hiyo cha  Mindanao Februari 9, 2018.



Rais wa Ufilipino, Rodrigo Duterte, amesema kuwa anataka wafanyakazi wa Kifilipino kuondoka nchini Kuwait ndani ya saa 72 baada ya mtumishi wa kazi za ndani raia wa Ufilipino kukutwa amekufa na kuwekwa ndani ya jokofu katika nyumba moja isiyokaliwa na watu katika taifa hilo la Ghuba.

Duterte amesema kuwa ameiagiza Wizara ya Kazi kufanya uratibu na mashirika ya ndege ya Ufilipino kuwapatia tiketi za bure wafanyakazi wa Kifilipino walioko nchini Kuwait ambao wanataka kurejea nyumbani.

"Ninataka waondoke (Kuwait), wale wanaotaka kuondoka, ndani ya saa 72," aliwaambia waandishi wa habari. "Tutahesabu uhai wetu kwa saa kwa sababu ni dhahiri kuwa kila saa moja Wafilipino wanafanyiwa mateso, dhulma na ukatili."

Mnamo mwezi Januari, Ufilipino ilisitisha zoezi la kupeleka wafanyakazi nchini Kuwait baada ya kutokea kwa vifo vyenye utata dhidi ya Wafilipino katika miezi ya hivi karibuni.

Duterte alisema kuwa marufuku hiyo itaendelea mpaka pale serikali itakapokuwa na uhakika kwamba kuna usalama kwa wafanyakazi nchini Kuwaita ambako Wafilipino 103 walifariki dunia mwaka 2017, kutoka watu 82 waliopoteza maisha mwaka 2016.


"Niko tayari kuchukua hatua kali zitakazosaidia kulinda uhai na maisha ya Wafilipino," alisema. "Hatuna nia ya kuikosea serikali yoyote au mtu yeyote. Lakini kama zuio linahitajika, basi liendelee tu."

"Zuio linaendelea sasa na sijui litaendelea mpaka lini," aliongeza.

Mnamo siku ya Jumanne, mwili wa mfanyakazi wa ndani mwenye umri wa miaka 29 aitwaye Joanna Daniela Demafelis ulikutwa ndani ya jokofu nchini Kuwait, ambako Wafilipino wapatao 250,000 wanafanya kazi na kuishi. Kwa mujibu wa Durtete, mwili wa mwanamke huo ulikuwa na alama za mateso na ilionekana kuwa amenyongwa.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment