GHANA YATUMA SATELAITI YAKE YA KWANZA ANGANI

satellite_space_communication-100613561-primary.idge 

Ghana imetuma angani satelaiti yake ya kwanza tangu ilipojipatia uhuru. Satelaiti hiyo ya GhanaSat 1, ilitengenezwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha All Nation cha nchini humo.

Kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini humo, GhanaSat-1, iliyorushwa kutoka kituo cha anga cha kimataifa, pamoja na mambo mengine itatumika kwa tafiti za sayansi na mafunzo ya masuala ya anga nchini humo na Afrika kwa ujumla.

Kwa mujibu wa mratibu wa mradi huo, Dk Richard Damoah, satelaiti hiyo pia itasaidia kutoa mafunzo kwa kizazi kichanga juu ya namna ya kutumia satelaiti kwenye shughuli mbalimbali katika bara zima.

Uzinduzi huo wenye mafanikio umeiweka Ghana kwenye ramani ya kimataifa kama nchi ya kwanza katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara kutuma  satelaiti ya kimafunzo angani.

Rais wan chi hiyo Akufo-Addo amekipongeza Chuo Kikuu cha All Nations University kwa kufanikisha mradi huo.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment