HATUA 5 RAHISI ZA KUJIWEKEA AKIBA

money_256312_640.jpg 

Baadhi ya watu huona ugumu kujiwekea akiba kwa sababu mbalimbali: kipato kisichotosheleza, kuongezeka kwa mahitaji ya nyumbani, gharama za biashara, madeni mengi au muda mfinyu wa kuangalia mipango ya uwekezaji iliyopo sokoni.

Lakini kipato chako hata kikiwa kidogo kiasi gani, hakuna kisingizio cha kuchelewa kuweka akiba. Unaweza kukuta ugumu kidogo katika jambo hili kwa sababu utahitaji kubadilisha mtindo wa maisha yako, lakini ina faida nyingi ambazo zinapaswa kukusukuma kulifanya.

Kuna njia kayaya za kujiwekea akiba, lakini kwanza unahitaji mpango. Hapa tunakuletea dondoo za kutengeneza mpango wa kuweka akiba:

1. ANZA MARA MOJA

Hakuna muda maalum wa kuanza kuweka akiba. Unapoamua kuweka akiba, anza mara moja kulingana na mpango wako.

2. TENGA KIWANGO CHA AKIBA

Fanya uamuzi wa kiwango fulani cha mapato yako ya kila mwezi unachotaka kuweka akiba. Kwa mfano umeamua kuweka asilimia 10. Ili kufanikisha kutoka kwenye 0 kwenda 10, unaweza kuanza kuweka asilimia 3 katika mwezi wa kwanza, kisha ongea kiwango hicho mpaka asilimia 6 baada ya miezi 3 na hatimaye ongeza mpaka asilimia 10 baada ya miezi sita. Kama una umri wa zaidi ya miaka 50, unaweza kuhitaji kutenga asilimia 20 ya kipato chako na kukiweka katika akiba yako.
  
3. JILIPE KWANZA

Unapopokea mshahara wako, punguza asilimia 10 kwanza kabla ya mambo mengine. Ikiwezekana, weka akiba yako kwenye akaunti maalum ya benki.

piggy_bank_390528_640.jpg


4. ONGEZA ZAIDI AKIBA YAKO

Ainisha gharama zako kulingana na mahitaji yako. Kiasi kinachobaki kiweke kwenye akaunti ya akiba yako. Unaweza kupunguza mahitaji yako, usisite kufanya hivyo. Ukipata mgao kwenye biashara yako mwishoni mwa mwaka, unaweza kuamua kujilipa kwa kuuweka mgao huo kwenye akiba yako.

5. FUATILIA MPANGO WAKO

Fuatilia maendelea ya akiba yako. Unaweza kuamua kuchukua kiasi fulani cha pesa yako na kukiwekeza kwenye biashara mbalimbali za uhakika kulingana na malengo yako. Iwapo mpango wako wa kuweka akiba hautaenda vizuri kwenye miezi ya mwanzo, usikate tamaa. Wakati fulani gharama halisi zinaweza kuvuka bajeti. Badala ya kukanganyikiwa, chunguza matumizi yako na uyarekebishe kulingana na mpango wako.


Inaweza kuchukua muda kufanya marekebisho kabla ya kufikia lengo lako. Kitu muhimu kabisa ni kuanza kutekeleza utaratibu huo wa kujiwekea leoleo.

Mzizima 24 WhatsApp: +255 626 603 852


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment