AJALI YA NDEGE YAUA WATU 61 KUSINI MWA URUSI

All sixty-two people on board a flight from Dubai were killed when the plane crashed and burst into flames as it was landing in Rostov-on-Don, in Southern Russia, on March 19 morning, a local official said. (AFP Photo) 


MOSCOW: Watu wote 61 waliokuwa kwenye ndege ya Shirika la Ndege la flydubai aina ya Boeing 737 wamepoteza maisha baada ya ndege yao kupata ajali na kuteketea kabisa wakati ikitua katika mji wa Rostov-on-Don, kusini mwa Urusi leo, maafisi wamesema.

Ajali hiyo imtokea wakati ndege hiyo ikijaribu kutua kwa mara ya pili lakini hali mbaya ya hewa ilifanya ikosee njia na kulipuka.

“flydubai inasikitika kuthibitisha kuwa ndege namba FZ981 imepata ajali wakati ikitua na kwamba tukio hilo la kusikitisha limesababisha vifo,” shirika hilo limesema kwenye ukurasa wake wa Facebook.

Wizara ya mambo ya dharura nchini humo imethibitisha kuwa abiria wote 55 na wafanyakazi 6 waliokuwa kwenye ndege wamepoteza maisha.

“Ndege aina ya Boeing 737 ilipata ajali wakati ikitua. Ilikuwa imebeba watu 61. Wote wamepoteza maisha”, amesema msemaji wa wizara hiyo kama alivyonukuliwa na shirika la habari la TASS.

Ndege hiyo iligonga chini mita mia moja kutoka eneo la kutua wakati ikijaribu kutua kwa mara ya pili.

Picha za video kwenye vyombo vya habari vya eneo hilo zimeonesha moto mkubwa ukiwaka kutoka kwenye eneo la ajali.


Mvua ilikuwa ikinyesha sana na tahadhari ya upepo mkali ilikuwa imetolewa na wizara ya dharura ya eneo hilo, shirika la habari la TASS limesema.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment