UINGEREZA YAANZA MASHAMBULIZI YA ANGA NCHINI SYRIA

Analysts say Britain could have to face serious backlashes if it launches air strikes against ISIL terrorists in Syria.

Uingereza imeripotiwa kuanza mashambulizi yake dhidi ya maeneo ya kundi la Dola la Kiislamu nchini Syria baada ya serikali kupata idhini ya bunge ya kufanya mashambulizi hayo.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, duru za serikali zimesema kuwa Uingereza imeanza mashambulizi yake ya ndege nchini Syria.

Serikali hiyo haijaweza wazi undani wa mashambulizi hayo, lakini ripoti za vyombo vya habari zimemnukuu Waziri wa Ulinzi wa Uingereza Michael Fallon akisema kuwa ndege zake zimeshambulia visima vya mafuta mashariki mwa Syria.

Hatua hiyo imefuatia mjadala mkali uliodumu kwa saa 10 mapema Jumatano, ambapo wabunge 397 walipiga kura kuiunga mkono huku wengine 223 wakipinga hatua ya Uingereza kupanua mashambulizi yake ya ndege kutoka Iraq mpaka Syria.

Kufuatia kura hiyo, Waziri Mkuu wa Uingereza aliusifu uamuzi huo kwa kuuita kuwa ni “uamuzi sahihi” akisema, “ninaamini bunge limechukua uamuzi sahihi wa kuendelea kuifanya Uingereza kuwa salama… hatua ya kijeshi nchini Syria ni sehemu ya mkakati wetu mpana.”

Cameron alikuwa miongoni mwa waungaji mkono wakubwa wa upanuzi wa mashambulizi ya anga ambayo ni sehemu ya ushirika unaoongozwa na Marekani dhidi ya maeneo yanayoshikiliwa na kundi hilo nchini Iraq.

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uingereza, Philip Hammond, aliikaribisha taarifa hiyo akisema kuwa Uingereza imekuwa “salama zaidi kwa sababu ya hatua iliyochukuliwa na wabunge”. Mashambulizi ya kijeshi pekee hataisaidia Syria, hatatufanya tuwe salama dhidi ya Daesh lakini. Lakini msimamo huu wa pamoja utatusaidia.”

Muda mfupi baada ya kura hiyo ya bunge, ndege za Uingereza ziliruka kutoka kambi ya jeshi la anga ya Akrotiri nchini Cyprus. Mahali zilikoelekea hapajulikani na watawala wa Uingereza hawakuwa tayari kulizungumzia.

Wakati wa mjadala bungeni, Cameron aliwataka wabunge kuitikia wito wa washirika wao na kuchukua hatua dhidi ya kundi la Dola la Kiislamu ambalo linataka kuwaua na kuwapachika kasumba watoto wao.

"Je, tushirikiane na washirika wetu kukabili kitisho hiki na kuwafuata magaidi hawa katika maeneo yao wanayopanga kuwaua Waingereza, au tukae na kutusubiri watushambulie?” alisema.

Kiongozi wa chama cha Labour, Jeremy Corbyn, alipinga hatua hiyo lakini akawapa uhuru wabunge wa chama chake kuiunga mkono au kuikataa.

Katika kujibu hotuba ya Cameron, Corbyn alisema, “Haiwezekani kuepuka hitimisho kuwa waziri mkuu anatambua upinzani wa umma dhidi ya wazo lake bovu la kukimbilia kwenye vita… na anataka kura ifanyike kabla mambo hayajamwendea kombo. Ni wazi kuwa mawazo ya waziri mkuu ya kuchukua hatua za kijeshi hayakubaliki”.

Katika andiko lake kwenye mtandao wa Facebook alililolichapisha baada ya kura ya bunge, Corbyn alirejea msisitizo wa kuutafutia mgogoro huo suluhisho la amani, akasema: “Nimekuwa nikisisitiza na nitaendelea kufanya hivyo kwamba, tunatakiwa kuongeza mara dufu juhudi za kutumia njia za kidplomasia na kisiasa kumaliza mzozo wa Syria.”

“Askari wa Uingereza watakuwa hatarini na upotevu wa maisha ya watu wasiokuwa na hatia hautakwepeka,” aliandika Corbyn.

Rais wa Marekani Barack Obama aliukaribisha uamuzi huo na kusema: “Tangu tulipoanza mapambano dhidi ya ISIL, Uingereza imekuwa miongoni mwa washirika wetu wa thamani kabisa katika mapambano hayo. Tunatarajia kuona vikosi vya Uingereza vikiungana na vikosi vya washirika katika anga ya Syria, na tutawajumuisha katika vikosi vya anga vya ushirika wetu haraka iwezekanavyo.”

Aidha, Obama aliusifu uamuzi wa hivi karibuni wa serikali ya Ujerumani kutuma askari 1,200 kushiriki mapambano dhidi ya ugaidi nchini Syria.

Tangu Agosti 2014, Marekani na baadhi ya washirika wake wamekuwa wakifanya mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo yanayokaliwa na kundi la Dola la Kiislamu nchini Iraq.

Baadhi ya washirika hao wamekuwa wakifanya hivyo nchini Syria bila idhini ya Damascus au Umoja wa Mataifa tangu Septemba mwaka jana.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment