SAMUEL ETO’O ATEULIWA KUWA KOCHA WA KLABU YA ANTALYASPOR

 index


Mshambuliaji wa zamani wa klabu za Barcelona, Chelsea, Inter Milan na Everton ameteuliwa kuwa kocha wa klabu ya Antalyaspor ya nchini Uturuki, baada ya kuondoka kwa kocha mkuu Yusuf Simsek. Mkongwe huyo wa Cameroon aliyejiunga na klabu hiyo mwezi Juni kwa mkataba wa miaka mitatu, alitaarifiwa na rais wa klabu hiyo kuchukua majukumu ya ukufunzi pamoja na mkurugezi wa ufundi Mehmet Ugurlu mpaka kocha mpya atakapoajiriwa.

"Tulikaa na [mkurugenzi wa ufundi] Mehmet Ugurlu na Eto'o. wote wawili wataungana katika mafunzo. Bodi imewapa Ugurlu na Eto'o jukumu la mafunzo mpaka kocha mpya atakapopatikana,” rais wa klabu, Gultekin Gencer aliliambia shirika la habari la DHA.

Kwa jukumu hilo jipya, sasa Eto'o atakuwa na majukumu mawili ya ukocha na kuwa mchezaji. Kwa sasa Eto’o ndiye mfungaji wa bora wa Super Lig akiwa na magoli 13 katika mechi zake 15 za mwanzo na Antalyaspor. Klabu imempa mshambuliaji huyo mechi tatu za kujithmini, kisha atathmini upya hali baada ya mapumziko ya ligi hiyo.

Mwaka 2005, Eto’o alishika nafasi ya tatu katika uteuzi wa FIFA wa mchezaji bora wa mwaka, na amewahi kuteuliwa mara nne kuwa mchezaji bora wa Afrika. Alishinda makombe mawili ya Michuano ya Mataifa ya Afrika, na ndiye mshindi wa taji la mfungaji bora wa michuano hiyo.

Mfungaji bora huyo wa timu ya taifa ya Cameroon, alishiriki katika makombe manne ya dunia, na makombe sita ya michuano ya mataifa ya Afrika.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment