BLATTER NA PLATINI WAPEWA KIFUNGO

This file photo, taken on June 11, 2014, shows FIFA President Joseph Sepp Blatter (L) talking to UEFA President Michel François Platini during the 64th FIFA congress in Sao Paulo, Brazil. (Photo by AFP)
Rais wa FIFA Joseph Sepp Blatter (kushoto) akizungumza na Rais wa UEFA Michel François Platini wakati wa mkutano wa 64 wa FIFA uliofanyika mjini Sao Paulo, nchini Brazil, Juni 11, 2014.



Shiriko la Soka Duniani (FIFA) limempiga marufuku rais wake, Joseph Sepp Blatter, na rais wa muungano wa vyama vya soka barani Ulaya (UEFA), Michel François Platini, kutojihusisha na shughuli za soka kwa miaka minane.

Kamati ya maadili ya Shirikisho hilo limewakuta wawili hao na hatia ya kutumia vibaya nafasi zao kufuatia malipo ya kitita kipatacho milioni mbili za franca za Uswizi (zaidi ya dola milioni mbili) kilichotolewa na Blatter mwaka 2011 kwenda kwa Platini.

Aidha, Blatter amepigwa faini ya franca 50,000 za Uswizi ($50,250), wakati  Platini akipigwa faini ya franca 80,000 ($80,400).

“Katika maelezo yake ya maandishi wala katika maelezo yam domo, bwana Blatter hakuweza kuonesha kuonesha msingi mwingine wa kisheria wa malipo haya. Kwa kushindwa kuweka mbele maslahi ya FIFA na kuacha kufanya jambo lolote ambalo linapingana na maslahi ya FIFA, Bwana Blatter alikiuka jukumu lake la kimaadili kwa FIFA,” walisema majaji.

Waliongeza kuwa, “Mada yake (Blatter) kuhusu makubaliano ya mdomo yalionekana kuwa hayana nguvu na kukataliwa na jopo.”

Aidha, majaji hao walisema kuwa Platini “alishindwa kutenda kulingana na uaminifu na uadilifu, na kuonesha kutojua umuhimu wa majukumu yake.”


Uamuzi wa jopo hilo la maadili lililoongozwa na Hans Joachim Eckert, umehitimisha vuta ni kuvute ya Blatter na Platini juu ya soka la kimataifa na kuondosha ndoto zao za kugombea urais wa FIFA katika uchaguzi utakaofanyika Februari 26 mwaka ujao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment