UHABA WAZIKUMBA SHULE BAADA YA WALIMU WA KIGENI KUTIMKA


Shule na vyuo binafsi vitakabiliwa na upungufu mkubwa wa walimu kuanzia mwaka ujao wa masomo kufuatia walimu wengi wa kigeni kuondoka nchini kutokana na kukosa vibali vya kazi.

Uondokaji wa walimu hao ni pigo kubwa kwa shule binafsi ambazo zinategemea sana walimu wa kigeni.

Chama cha Waendeshaji na Wamiliki wa Shule na Vyuo visivyokuwa vya kiserikali (Tamongsco) jana kilielezea wasiwasi huo na kusema kuwa kwa uchache walimu 3,400 wameshaondoka nchini.

“Kutokana na uondokaji huu, ndani ya wiki mbili zijazo shule hazitakuwa na walimu wa kigeni,” katibu mkuu wa Tamongsco, Benjamin Nkonya, aliiambia the The Citizen jana jijini Dar es Salaam.

Hilo limetokea kufuatia agizo la serikali linalowataka waajiri wote kuhakikisha waajiriwa wao wasiokuwa raia wanafanya kazi kihalali kwa kuwapatia vibali vya kazi badala nyaraka za muda (CTA).

Katika tangazo hilo, serikali imetoa muda wa mpaka mwishoni mwa mwezi huu kwa waajiri kufuata sheria ya ajira kwa raia wa kigeni kwa kuhakikisha wanawapatia vibali vya kazi wafanyakazi wao.

Kwa sasa, gharama ya kibali cha kazi ni dola 2,500 (takriban milioni 5) ambayo, kwa mujibi wa bwana Nkonya, shule hizo haziwezi kumudu.

Ingawa hakuzitaja shule ambazo zimeathirika, alisema kuwa nyingi ni za mikoa ya Dar es Salaam, Kilimanjaro, na Kagera. Wageni wanaofanya kazi katika shule binafsi nchini wengi wao wanatoka katika nchi za Kenya, Uganda, Malawi, na Rwanda.

Akielezea suala hilo, katibu mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Prof Sifuni Mchome, amesema kuwa suala hilo liko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Hata hivyo, alisema ingawa nchi ilikuwa na upungufu wa walimu wa sayansi, mchakato wa kuwaajiri wa kigeni ulipaswa kufuatwa, wakati Tamongsco ikiendelea kuishawishi serikali kuondoa ada ya vibali vya kazi.

Katibu mkuu huyo alibainisha kuwa nchi inakabiliwa na upungufu wa walimu 27,000 wa masomo ya sayansi, na kwamba lilikuwa jambo jema kuwaajiri kutoka nje ya nchi.

Prof Mchome alisema kuwa Tamongsco ilijaribu, bila mafanikio, kufuatilia ombi lake la kuitaka serikali iondoa ada ya vibali vya kazi ambayo iliwekwa kwa walimu wa kigeni.


CHANZO: The Citizen
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment