ERDOĞAN: UTURUKI INA USHAHIDI KUWA URUSI INAHUSIKA NA MAFUTA YA DAESH

 

RAIS  wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan mapema leo amesema kuwa nchi hiyo ina ushahidi kwamba Urusi inajihusika na biashara haramu ya mafuta kutoka kundi la Dola ya Kiislamu  nchini Syria (ISIS), hali inayoonekana kama majibu dhidi ya tuhuma za Urusi kwamba Uturuki inanunua mafuta kutoka kundi hilo.

Jana Jumatano wizara ya ulinzi ya Urusi ilimtuhumu Erdoğan na familia yake kuhusika na biashara hiyo baada ya Ankara kutungua ndege ya kivita ya Moscow mwezi uliopita jambo lililouzamisha uhusiano wa nchi hizo katika mgogoro.

"Katika siku za hivi karibuni umeibuka mtindo unaoongozwa na Urusi. Hakika, hata Urusi haiamini hili pia,” alisema Erdoğan, akikusudia tuhuma za kuhusika na baishara ya mafuta kutoka kwa kundi hilo.

"Tazama, Urusi inatakiwa kuthibitisha kuwa Jamhuri ya Uturuki inanunua mafuta kutoka kwa kundi la Daesh, vinginevyo haya ni masingizio,” alisema, huku akisisitiza kuwa atajiuzulu iwapo Urusi itaweza kuthibitisha madai hayo.

"Nani anayenunua mafuta kutoka kwa Daesh? Ngoja niseme. George Haswani, mwenye pasipoti ya Urusi na uraia wa Syria, ni miongoni mwa wafanyabiashara wakubwa wa shughuli hizi,” alisema Erdoğan.

Mwezi Novemba, Wizara ya Fedha ya Marekani ilimuwekea vikwazo Haswani, ambaye pia aliwekwa kwenye orodha ya vikwazo ya Muungano wa Ulaya, kwa kufanya kazi kama mtu wa kati kwa ajili ya ununuzi wa mafuta unaofanywa na serikali ya Syria kutoka kundi hilo la Daesh (ISIS).


Erdoğan amesema “mchezaji maarufu wa santaranji kutoka Urusi” anahusika pia na biashara hiyo ya mafuta, bila kumtaja jina. “Naye yumo katika mashindano haya,” alisema.

Aidha, vikwazo vya Marekani vilimkumba Kirsan Ilyumzhinov, tajiri wa Kirusi na rais wa muda mrefu wa Shirikisho la Mchezo wa Santranji Duniani (FIDE) ambaye aliwahi kuwa mkuu wa jimbo la Kalmykia kusini mwa Urusi.

Jumatano Marekani ilikanusha madai ya Urusi kwamba Uturuki inahusika na ununuaji wa mafuta ya Daesh.

Josh Earnest, msaidizi wa rais na msemaji katika Ikulu ya ametupilia mbali madai hayo na kumlaumu Assad kuwa anahusika na biashara ya mafuta kutoka kundi hilo.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment