VIONGOZI WA MAPINDUZI BURKINA FASO WAAMURIWA KUJISALIMISHA

Demonstrators shout slogans next to burning tree branches in the Tampouy neighborhood of the capital Ouagadougou during a protest on September 21, 2015. (AFP photo)
Waandamanaji katika mji mkuu wa Burkina Faso, Ouagadougou jana Septemba 21, 2015.



Wakuu wa kijeshi nchini Burkina Faso wamewaamuru askari wa kikosi cha ulinzi wa rais, kilichofanya mapinduzi dhidi ya serikali ya mpito wiki iliyopita, kuweka silaha zao chini.

Katika taarifa iliyotolewa jana Jumatatu, wakuu hao wa kijeshi wamewatolea wito wanamapinduzi hao kuzisalimisha silaha zao kwenye kambi za jeshi kwa ahadi ya kudhamini usalama wao.

Wamesema kuwa vikosi vya taifa hilo vinaelekea katika mji mkuu, Ouagadougou, kutoka mikoani kwenda kuwanyang’anya silaha askari wa kikosi cha ulinzi wa rais bila kumwaga damu.

"Vikosi vyote vya taifa vinaelekea Ouagadougou kwa lengo moja la kuwapokonya silaha kikosi cha ulinzi wa rais (RSP) bila kumwaga damu,” ilisema taarifa hiyo na kuongeza, "Tunawataka wajisalimishe."

Mapinduzi hayo yalifanywa na Jenerali Gilbert Diendere, mshirika wa karibu wa aliyekuwa Rais Blaise Compaore, ambaye aliondolewa madarakani mwaka jana kufuatia maandamano ya kuipinga serikali yake baada ya kutaka kufanya jaribio la kubadili katiba ili kubaki madarakani.

Viongozi wa mapinduzi mapya wametangaza kulivunja bunge na serikali ya mpito ambayo ilipewa jukumu la kuongoza kipindi cha mpito baada ya kung’olewa kwa Compaore mwaka jana.

Jenerali Diendere ametawazwa kuwa kiongozi mpya wa Burkina Faso licha ya hatua hiyo kulaaniwa vikali na nchi za Magharibi na Umoja wa Afrika (AU).

Serikali ya mpito iliyokuwa ikiongozwa na Kafando ilikuwa imepanga tarehe 11 Oktoba kuwa tarehe ya kufanyika uchaguzi wa rais na wabunge, ambao ungekuwa wa kwanza tangu Compaore alipoondolewa madarakani.

Kwa uchache watu 10 wamepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mfululizo wa ghasia tangu yalipofanyika mapinduzi hayo.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment