TOTTENHAM YAMTEMA ADEBAYOR

Straika wa Tottenham Hotspur Emmanuel Adebayor wakati wa mechi dhidi ya Stoke City kwenye uwanja wa White Hart Lane mjini London Desemba 22, 2012



Mshambuliaji wa Togo Emmanuel Adebayor amefunguliwa mlango wa kuondoka Tottenham Hotspur kwa makubaliano yaliyofikiwa baina ya pande mbili, klabu hiyo imetangaza leo.

Kuondoka kwa straika huyo mwenye umri wa miaka 31 kulitarajiwa baada ya kutojumuishwa katika kikosi cha wachezaji 25 wa Tottenham katika Ligi Kuu msimu huu au kupewa namba.

"Tunaweza kuthibitisha kuwa tumefikia makubaliano na Emmanuel Adebayor ambayo yatamruhusu kuondoka klabuni,” Spurs wamesema katika taarifa iliyowekwa kwenye tovuti yao. “Tunamtakia Emmanuel kila la heri katika mustakbali wake.”

Adebayor aliyewahi kuchezea klabu za Metz, Monaco, Arsenal, Manchester City na Real Madrid, alijiunga Spurs kwa mkopo mwaka 2011, kisha akasaini mkataba wa kudumu Agosti 2012.

Mwaka 2011 - 2012 alikuwa mfungaji bora wa Spurs akiwa na magoli 18, lakini mwaka 2013 meneja Andre Villas-Boas alimwambia afanye mazoezi na timu ya vijana ya klabu hiyo.

Kuteuliwa kwa Tim Sherwood kama mrithi wa Villas-Boas kulimuibua tena Adebayor kwa muda mfupi, lakini alianza kutoonekana sana baada ya Mauricio Pochettino kuchukua mikoba ya kuifundisha klabu hiyo msimu uliopita, akionekana mara 10 tu.

"Nilikuwa muwazi kwake. Tulifanya mazungumzo kabla ya msimu uliopita kufikia kikomo na nilimwelezea wazo langu,” Pochettino alisema juzi Ijumaa.

"Nadhani iko wazi kuwa hayuko akilini mwangu au katika mipango ya baadae ya Tottenham. Si tatizo kwake wala kwetu.

"Ilikuwa wazi tokea mwanzo, miezi mitatu au minne iliyopita, na alikuwa na uamuzi wa kubaki au kuondoka.


"Muda wote tuko tayari kumsaidia. Tuna uhusiano mzuri. Tatizo pekee kwa sasa ni kutafuta ufumbuzi kwake na kwa klabu, jambo ambalo ni zuri kwa pande zote mbili.”


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment