SKENDO YA UFISADI YAMNG’OA RAIS WA GUATEMALA

Guatemalan President Otto Perez Molina (Photo by AFP)
Rais wa Guatemala Otto Perez Molina



RAIS wa Guatemala, Otto Perez Molina, amejiuzulu muda mfupi baada ya kutolewa kibali cha kukamatwa kufuatia skendo ya ufisadi ulioitikisa serikali yake.

Kiongozi huyo ameamua kung’atuka madarakani ili kupambana yeye mwenyewe dhidi ya mashitaka yanayomkabili, amesema msemaji wake Jorge Ortega.

Kung’atuka huko kumekuja saa chache baada ya jaji kutoa kibali cha kukamatwa wakati mashitaka yakiandaliwa dhidi ya tuhuma za ufisadi zinazodaiwa kufanywa na utawala wake.

Kutokana na amri hiyo ya mahakama, Perez Molina atalazimika kufika mbele ya jaji Miguel Angel Galvea kujibu mashitaka ya matumizi mabaya ya madaraka, ukwepaji kodi na upokeaji rushwa.

Mapema juzi Jumanne, Bunge la nchi hiyo lilimuondolea kinga ya kutoshitakiwa na hivyo kuandaa mazingira ya kushitakiwa kwa tuhuma za kuhusika na mpango wa kifisadi ambao wafanyabiashara wanaripotiwa kuwa walitoa hongo ili kukwepa ushuru wa forodha.

Perez Molina mwenye umri wa miaka 64, amekanusha tuhuma hizo na kuahidi kukabiliana na mkondo wa sheria. Mpaka sasa hakuna mashitaka yaliyowasilishwa dhidi yake.

Hii ni mara ya kwanza katika historia ya nchi hiyo kwa rais aliye madarakani kufikishwa mbele ya sheria.


Viongozi wa wafanyabiashara, Baraza la Maaskofu wa nchi hiyo na hata ofisi ya mdhibiti wa mahesabu ya serikali walikuwa wamemtaka Perez Molina kujiuzulu.

Soma zaidi kuhusu skendo hiyo>>>http://www.mzizima24.com/2015/09/guatemala-yamzuia-rais-kusafiri-nje-ya.html
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment