NITAZUNGUMZIA HAKI ZA MASHOGA, ASEMA OBAMA

 President Obama in a past address

Rais wa Marekani Barack Obama amesema kuwa atatetea msimamo wake juu ya haki za mashoga kufuatia upinzani wa suala hilo unaoendelea nchini Kenya.

Akizungumza na shirika la habari la BBC, Rais Obama amesema kuwa atazungumza bila kificho dhidi ya ufisadi na ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa ziara yake nchini humo.

“Mimi si shabiki wa ubaguzi na uonevu kwa yeyote kwa msingi wa rangi, dini au jinsia,” alisema.

Obama amekosolewa vikali nchini Kenya kufuatia hatua yake ya kuunga mkono haki za mashoga huku viongozi wengi wa Kenya wakimuonya dhidi ya kuibua suala hilo wakati wa ziara yake.

Viongozi hao, wakiongozwa na Naibu Rais William Ruto, wamezungumzia msmamo wa wazi wa nchi hiyo kupinga ndoa za jinsia moja na kwamba watapinga sheria yoyote itakayolenga kuhalalisha ndoa za mashoga.

Akizungumza katika kanisi la AIC mjini Nairobi Bwana Ruto alionya kwamba sheria yoyote itakayolenga kuruhusu ushoga nchini humo itapingwa vikali na kuzuiliwa.

“Ushoga ni kinyume na mpango wa Mwenyezi Mungu na haupaswi kuvumiliwa. Mungu hakuumba mwanaume na mwanamke ili wanaume wawaoe wanaume na wanawake wawaoe wanawake wenzao.”

Wakati wa ziara yake nchi Senegal mwaka 2013, Obama alizitolea wito serikali za Afrika kutoa haki sawa kwa mashoga kwa kuacha kutunga sheria zinazowabagua.

Mpaka sasa Afrika Kusini ndio nchi pekee ya Kiafrika iliyohalalisha ushoga.

Obama anatarajiwa kuizuru Kenya kuhudhuria Mkutano wa Kilele wa Ujasiriamali Duniani (GES) unaotarajiwa kuanza leo Julai 24 mpaka 26 jini Nairobi, na anatarajiwa kufanya mazungumzo na Rais Uhuru Kenyatta kuhusu uhusiano wa nchi hizo mbili.

Obama atakuwa rais wa kwanza wa Marekani aliye madarakani kuhutubia mkutano wa Umoja wa Afrika atakaposafiri kwenda Ethiopia siku ya Jumapili.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment