MTOTO WA SIKU MOJA ATOWEKA HOSPITALI


Up to 300,000 Spanish babies were stolen from

Musoma. Mama mmoja amechanganyikiwa baada ya mwanaye wa siku moja kuibiwa na mtu asiyejulikana katika Hospitali ya Rufaa mkoani Mara.

Mama huyo, Msuba Elias,17, alisema kuwa kwenye majira ya saa 2 asubuhi mwanamke mmoja alikwenda moja kwa moja kwenye kitanda chake na kumuuliza jina lake. Kisha alimwambia kuwa nesi katika wodi namba nane alikuwa akimuita.
Baada ya kufika kwa nesi aliyedaiwa kumuita, alikataa. Alirudi wodini lakini alishtuka baada ya mwanaye kutokuwa kitandani. Alimuuliza mama mwingine aliyekuwa amelala kwenye kitanda cha jirani akamwambia kuwa mwanaye alichukuliwa na mtoto mmoja.

Alimtafuta mwanaye katika maeneo mbalimbali hospitalini hapo bila mafanikio, ndipo aliposhauriwa kuliripoti suala hilo katika kituo kikuu cha polisi mjini Musoma.


Kwa mujibu wa Bi. Musiba, alibeba ujauzito alipokuwa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Iyovu wilayani Bukombe, mkoani Geita.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara Philip Kalangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa taarifa ya kina itatolewa baadaye kwa waandishi wa habari.

CHANZO: The Citizen


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment