MAZISHI YASITISHWA BAADA YA MAITI KUTABASAMU

 baby `rises from the dead' in Nyamira

Wakazi wa kijiji cha Bundo katika Kaunti ya Nyamira nchini Kenya bado wapo katika hali ya utata mkubwa baada ya shughuli moja ya mazishi kusitishwa kufuatia tukio la mchanga ‘kufufuka’.

Kwa mujibu wa mtandao wa habari wa Citizen Digital, baba wa mtoto huyo anasema kuwa siku ya Jumapili mkewe aliyekuwa na ujauzito wa miezi saba alijifungua mtoto ambaye hajakomaa na baadaye kupelekwa katika hospitali ya Nyamira kwa matibabu.

Aliongeza kuwa mtoto huyo aliwekwa katika chumba cha watoto mpaka jana Jumanne ambapo wauguzi wa hospitali hiyo walitangaza kuwa mtoto huyo amekufa, jambo lililopelekea familia kuandaa taratibu za mazishi.

Mambo yalibadilika baada ya mwanamke mmoja kuomba auone mwili wa mtoto huyo ili atoe heshima zake za mwisho lakini akashtuka kuona ‘maiti’ ikitabasamu ndani ya jeneza.


Mama wa mtoto huyo ambaye alishtushwa na taarifa hizo na ambaye bado yuko hospitali, alielezea furaha yake baada ya kuambiwa kuwa mwanaye bado yu hai.

CHANZO: Citizen Digital
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment