KUTANA NA KIKONGWE WA MIAKA 101 ANAYEMHUDUMIA MWANAYE WA MIAKA 63

A mother's love is so strong 



Mama mmoja nchini Malaysia, Madam Meliah Diah, anakadiriwa kuwa na umri wa miaka 101 na anaweza kuonekana kuwa mtu aliyedhoofika sana, lakini hilo halimzuii kumtunza na kumhudumia mwanaye mlemavu mwenye umri wa miaka 63, Abdul Rahman Saud.
Kwa mujibu wa mtandao wa habari wa Harian Metro, mjane huyo ambaye kwa sasa anaonekana kama ishara na nembo ya upendo wa mama, ameendelea kumlea mwanaye huyo akiwa peke yake baada ya mumewe kufariki dunia miaka 22 iliyopita.

Anamlisha, kumuogesha, kumsafisha na kumuweka juani kila siku.

Taarifa hiyo inaongeza kuwa kuwa kila siku asubuhi, Madam Meliah humuogesha kwenye varanda la nyumba yao ya miti katika kijiji cha Bukit Nambua, katika mji wa Kedah. Akimaliza kumuogesha humlisha na kukaa hapo kwa siku nzima kabla ya kumrudisha ndani wakati wa jioni.

Diah amuambia mtandao wa Metro:

"Matatizo ya kifafa yaliyomkumba akiwa mdogo yamemfanya awe hivi. Muda wote anakuwa amelala kifudifudi na kusogea kidogo kidogo.

Anapenda kula wali. Tuko peke yetu, hatuna mtu mwingine. Ninatumai kuwa nisifariki dunia kabla yake kwa sababu hakuna mtu atakayemhudumia na kumtunza.”


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment