RIEK ATOA VITISHO KUMUONDOSHA KWA NGUVU RAIS SALVA KIIR

Riek Machar
Riek Machar



Kiongozi wa waasi Sudan Kusini Riek Machar ametishia kuandaa mapinduzi dhidi ya Rais Salva Kiir iwapo atakaa kuondoka madarakani mpaka kufikia usiku wa leo.

Machar amewaambia waandishi wa habari mjini Nairobi nchini Kenya kuwa mhumula wa utawala wa Kiir unafikia tamati usiku wa leo na kumtaka ajiuzulu kwa heshima ili kupisha mchakato wa uchaguzi.

Anautuhumu utawala wa Rais Kiir kwa kujaribu kufanya mabadiliko ya katiba ili kujiongezea muhula wa kukaa madarakani isivyo halali.

Akizungumza na mkutano huo wa wanahabari, Machar alionya kuwa iwapo Kiir hataondoka madarakani, wananchi wa Sudan Kusini watakuwa na kila haki ya kufanya uasi na kuuondosha kwa nguvu utawala wake.

Ametoa vitisho hivyo katika kilele cha maadhimisho ya 4 ya uhuru wa taifa hilo kutoka Jamhuri ya Sudan.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment