ASKARI 60 WA MISRI WAUAWA KATIKA ENEO LA SINAI

Egyptian emergency personnel move a victim into an ambulance following a car bomb explosion that targeted a police station in North Sinai’s provincial capital of el-Arish, April 12, 2015. (© AFP)
Wahudumu wa huduma za dharura wakimuingiza muathirika katika gari ya wagonjwa kufuatia mlipuko wa bomu kwenye kituo kimoja cha polisi katika mkoa wa kaskazini wa Al-Arish Aprili 12, 2015.

Kwa uchache askari 60 wa Misri wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mfululizo wa mashambulizi yaliyofanywa na wanamgambo kwenye vizuizi vya kijeshi katika eneo la Peninsula ya Sinai linaloendelea kushuhudia mawimbi ya ghasia.

Duru za kijeshi zinasema kuwa wapiganaji hao walilipua gari lililojazwa milipuko kusini mwa mji wa Sheikh Zuweid, kilometa 334 (maili 214) kaskazini mashariki mwa mji mkuu, Cairo, leo Jumatano, na kuwaua makumi ya askari huku wengine kadhaa wakijeruhiwa.
Kwa mujibu wa televisheni ya Sky News Arabia, washambuliaji hao pia walifanya mashambulizi kwenye vizuizi vya kijeshi katika wilaya za al-Joureh, Abu Refaei na  Sedrah kwenye viunga vya kusini vya mji wa Sheikh Zuweid.

Milipuko hiyo ilifuatia ufyatulianaji wa risasi baina ya vikosi vya serikali ya Misri na wapiganaji hao.

Wakati huo huo, waasi waiopungua 10 wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya helkopta za jeshi la Misri kushambulia maficho yao katika Peninsula ya Sinai.

Hatua hiyo inakuja zikiwa zimepita siku kadhaa baada ya waasi wasiopungua 11 kuuawa na wengine kukamatwa wakati askari wa serikali walipoyashambulia maficho ya wanamgambo hao katika mji wa Sheikh Zuweid na katika mji wa mpakani wa Rafah, kilometa 340 (maili 211) mashariki mwa Cairo.


Picha ya maktaba ikiwaonesha wanamgambo wa kundi la Wilayat Sinai, ambao zamani walijulikana kama Ansar Bait al-Maqdis, katika eneo la Peninsula ya Sinai.


Jeshi la Misri linaliona eneo la Peninsula ya Sinai kuwa kichaka cha wanamgambo.


Wanamgambo hao wamezidisha mashambulizi tangu Mohamed Morsi, rais wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia, alipopinduliwa na jeshi mnamo Julai 2013.


Wanamgambo kutoka kundi la Wilayat Sinai, ambao zamani walijulikana kama Ansar Bait al-Maqdis, wamedai kuhusika na mashambulizi mengi katika Peninsula ya Sinai. 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment