21 WAPOTEZA MAISHA NCHINI INDIA

The photo shows houses ruined by landslides in India’s Darejeeling, July 1, 2015.
Nyumba zilizoharibiwa vibaya na maporomoko ya ardhi katika mji wa Darejeeling, nchini India, Julai 1, 2015.


Kwa uchache watu 21 wamepoteza maisha katika maporomoko ya udongo yaliyosababishwa na mvua kubwa katika jimbo la Bengal nchini India.

Kwa mujibu wa polisi, kadhia hiyo imeiathiri miji ya Mirik, Kalimpong, na Darjeeling.


Aidha, imeripotiwa kuwa zaidi ya nyumba 100 na barabara vimeharibiwa vibaya katika miji hiyo.


Kadhia hii inatokea wiki moja baada ya watu wasiopungua 55 kupoteza maisha katika mafuriko na maporomoko ya ardhi yaliyolikumba jimbo la Gujarat magharibi mwa India.



Mafuriko la maporomoko ya ardhi ni matukio yanayolikumba eneo la Asia ya Kusini kila mwaka katika msimu kama huu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment