AMISOM YASHUTUMIWA KUUA RAIA

 African Union troops

Askari kutoka kikosi cha Umoja wa Afrika (AU) nchini Somalia, AMISOM, wamekosolewa kufuatia mfululizo wa vifo vya raia nchini Somalia.

 Vyombo vya habari na wahudumu wa afya nchini humo wanawatuhuma askari wa AU kwa kuua raia wasiopungua 22 ambao wamedai kuwa hawakuwa na silaha.

Tukio hilo linadaiwa kutokea katika mji wa Marka, kusini mwa Somalia.

Kwa mujibu wa kituo cha habari cha Al Jazeera, askari wa AU waliwafyatulia risasi vijana wasiokuwa na silaha waliokuwa wakicheza mpira.

Wakazi kadhaa walikimbia kuepuka mzozo huo. AMISOM imekanusha vikali madai hayo na kuweka ujumbe kwenye mtandao wa Twitter unaokanusha kutokea kwa tukio hilo.

Katika taarifa yake iliyotolewa Julai 21, 2015, AMISOM imesema kuwa askari wake walikutana na wapiganaji wa Al Shabaab na kuwaua wapiganaji watano.


Zaidi ya askari 20,000 kutoka mataifa kadhaa ya Afrika wanaunda kikosi cha AMISOM. Kikosi hicho kinapambana na wanamgambo wa Al Shabaab nchini Somalia.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment