WATANO WAPOTEZA MAISHA KATIKA MILIPUKO YA MABOMU MJINI BEIRUT

Lebanese security forces and firefighters gather at the site of twin bomb explosions that hit the Iranian Embassy in Beirut on November 19, 2013.
Eneo ilipotokea milipuko ya mabomu katika Ubalozi wa Iran mjini Beirut, Lebanon, Novemba 19, 2013.



Kwa uchache watu watano wamepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mashambulizi mawili ya bomu kusini mwa mji mkuu wa Lebanon, Beirut.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka nchini humo, mashambulizi hayo yametokea kusini mwa kiunga cha Bir Hassan jirani na Kituo cha Utamaduni cha Iran na Ubalozi wa Kuwait.

Kikundi cha Brigedi ya Abdullah Azzam kimedai kuhusika na milipuko hiyo kikisema kuwa kitaendelea kufanya mashambulizi dhidi ya maslahi ya Iran na kundi la Hizbollah nchini humo.

Katika miezi ya hivi karibuni, Lebanon imekuwa ikikumbwa na mashambulizi kama hayo, ambapo idadi kubwa ya watu wamepoteza maisha yao.

Zaidi ya watu 20, akiwemo mwambata wa Ubalozi wa Iran mjini Beirut, waliuawa na wengine wasiopungua 150 kujeruhiwa mwezi Novemba mwaka jana baada ya milipuko miwili kupiga jirani na ubalozi wa Iran kusini mwa mji huo.

Kufuatia tukio hilo, kundi la Brigedi ya Abdullah Azzam lilidai kuhusika na milipuko hiyo.

Kiongozi wa kundi hilo, Majid al-Majid, alikamatwa mapema Januari mwaka huu na kufariki dunia siku chache baadaye akiwa gerezani nchini Lebanon kutokana na kile kilichoelezwa kuwa ni kuzorota kwa afya yake.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment