MKUU WA JESHI LA COLOMBIA AFUTWA KAZI KWA KUIHUJUMU MAHAKAMA

Picture taken on January 20, 2014, shows Colombian Army Chief, General Leonardo Barrero, delivering a speech during a press conference in Tame Arauca, Colombia.
Jenerali Leonardo Barrero.


Rais wa Colombia, Juan Manuel Santos, amemfuta kazi mkuu wa majeshi wa nchi hiyo kwa matamshi ya kuishushia hadhi mahakama.

Jana Rais Santos alisema kuwa Jenerali Leonardo Barrero alikuwa amefutwa kazi kutokana na kauli yake ya utovu wa heshima dhidi ya mahakama na taifa kwa ujumla katika mazungumzo ya simu yaliyochapishwa mwishoni mwa wiki.

Tuhuma hizo zilichapishwa na jarida la Semana la nchini humo. Matamshi ya Barrero yalinaswa kwa siri wakati akizungumza na simu kuhusu upelelezi wa tuhuma za ufisadi uliokuwa ukifanywa na waendesha mashitaka.

Barrero alisikika akiwatukana waendesha mashitaka wakati akizungumza na kanali mmoja juu ya uwezekano wa kuhusika na mauaji ya kiholela.

Barrero alimwambia kanali Robinson Gonzalez del Rio, ambaye anakabiliwa na mashitaka ya jinai ya mauaji ya watu wawili mwaka 2007, kwamba waendesha mashitaka wanaochughuza mauaji hayo ni “kundi la wapuuzi” na kushauri kuwa yeye na wenzake “watengeneze mpango” wa kuwadhoofisha.

Baadhi ya maofisa wa jeshi wanatuhumiwa kuchukua hongo ya mpaka asilimia 50 ya mikataba, wengine wanatuhumiwa kuhamisha fedha zilizopangwa kutumika kwa ajili ya kambi na ugavi wa zana za jeshi.

Kwa mujibu wa ripoti ya jarida hilo la Semana, baadhi ya pesa zilipelekwa kwenye mifuko ya maafisa wanaotuhumiwa kufanya mauaji ya kiholela.

Serikali ya nchi hiyo imetangaza kuwa mnadhimu wa jeshi, Jenerali Juan Pablo Rodriguez, atachukua nafasi ya Barrero.

Tukio hilo limekuja wiki mbili baada ya baadhi ya vyombo vya habari kufichua kuwa kuna baadhi ya maafisa wamekuwa wakiwafanyia ujasusi wasuluhishi wa mazungumzo ya amani baina ya serikali na waaasi wa FARC.


Jeshi la Colombia limekuwa likipambana na waasi hao kwa miongo mitano sasa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment