WAANDAMANA KUPINGA BEI YA UMEME

This file photo shows thousands of South African civil servants marching through Pretoria.
Maelfu ya wafanyakazi wa sekta ya umma wakiandamana mjini Pretoria, Afrika Kusini.

Waandamanaji nchini Afrika Kusini wamefanya ghasia na kuzichoma moto nyumba kadhaa mashariki mwa mji mkuu wa nchi hiyo, Pretoria wakapinga kuapndishwa kwa bei za umeme.

Maandamano hayo yamekuja siku moja baada ya mkusanyiko mwingine katika eneo hilo kugeuka na kuwa wa ghasia, ambapo watu kadhaa walikamatwa, kwa mujibu wa duru za polisi na za wanausalama.

Polisi wanasema kuwa waandamanaji wanaodai kushushwa kwa bei za umeme walichoma ukumbi, kliniki na nyumba moja katika wilaya ya Bronkhorstspruit. Hata hivyo, taarifa ya jeshi hilo inasema kuwa hakuna aliyejeruhiwa katika matukio hayo.

Hilo ni tukio jipya kabisa katika mfululizo wa ghasia ambazo huzuka mara kwa mara katika maeneo ya jamii masikini nchini humo ambao wanaghadhibishwa na huduma duni zinazotolewa na serikali.

Wiki iliyopita waandamanaji walikichoma moto kituo kimoja cha polisi na ofisi za manispaa.

Wakaazi hao wamekuwa wakilalamika kuwa hawawezi kulipia gharama kubwa za umeme. Pia wanazilaumu mamlaka kwa kuzimbambikia bili familia zenye kipato cha chini.

Licha ya kuwa na utajiri wa madini na rasilimali za kilimo, kama ilivyo kwa nchi nyingi za Kiafrika, nchi hiyo bado imeendelea kuwa na viwango vidogo vya mishahara kwa wananchi.

Afrika Kusini ina hazina kubwa ya madini mbalimbali kama vile dhahabu, almasi, urania, makaa ya mawe na mengineyo.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment