UKRAINE YAKUMBWA NA MAAFA ZAIDI

Anti-government protesters holding makeshift shields throw tires during clashes with Ukrainian police in the capital Kiev on February 20, 2014.
Waandamanaji wakikabiliana na polisi katika mji mkuu wa Ukraine, Kiev leo Februari 20, 2014.



Kwa uchache watu 25 wamepoteza maisha nchini Ukraine katika makabiliano mapya baina ya Polisi na waandamanaji wanaoipinga serikali na kufanya idadi ya vifo kufikia zaidi ya watu 50.

Ghasia hizo ziliibuka baada ya wandamanaji waliojihami kuvamia vizuizi vilivyowekwa na polisi katika mji mkuu wa nchi hiyo, Kiev.

Waandamanaji wameudhibiti uwanja Maarufu wa Maidan (Uwanja wa Uhuru) katika mji huo, ambapo maelfu ya waandamanaji wamegoma kuondoka.

Hivyo ni vifo vipya kabisa kuanza kwa wiki hii, ambapo ghasia ziliibuka baada ya kwisha kwa muda wa mwisho uliowekwa na mamlaka za usalama zikiwataka waandamanaji kuondoka.

Ghasia hizo mpya zimekuja licha ya kuwepo kwa makubaliano baina ya Rais Viktor Yanukovych na viongozi wakuu wa upinzani.

Rais Yanukovych alitangaza mapatano hayo usiku wa kuamkia leo katika juhudi za kujaribu kuikwamua nchi hiyo.

Wakati huo huo, Mawaziri wa Mambo ya Nje kutoka Ufaransa, Ujerumani na Poland wamekuwa wakiendesha mazungumzo ya kutanzania mgogoro huo mjini Kiev.

Maafisa wa Ulaya wanasema kuwa wanafikiria kuchukua hatua za vikwazo dhidi ya serikali ya Ukraine kutokana na mgogoro huo.


Marekani imeweka vikwazo vya kuwapatia pasi za kusafiria maafisa waandamizi 20 wa Ukraine ambao wanadaiwa kutenda au kutoa maagizo ya ukiukwaji wa haki za binadamu katika ghasia hizo.

Kwa upande mwingine, Urusi imeyataka makundi ya upinzani nchini Ukraine kuacha ghasia na kukaa katika meza ya mazungumzo na serikali ili kutafuta ufumbuzi wa mgogoro huo kwa njia ya amani.

Ukraine ilikumbwa na maandamano dhidi ya serikali baada ya Rais Yanukovych kukataa kusaini Mkataba wa Ushirikiano na Umoja wa Ulaya Novemba 29, 2013, na badala yake akasaini mkataba wa kibiashara nan chi ya Urusi.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment