SASA NI RASMI: FACEBOOK KUINUNUA WHATSAPP KWA DOLA BILIONI 16

Mark-zuckerberg2
Mwanzilishi wa Facebook, Mark Zuckerberg 



Facebook imeingia makubaliano ya kuinunua WhatsApp, kwa dola bilioni 16, imefahamika.

Mkataba huo ndio mkubwa zaidi kuwahi kufanywa na Facebook mpaka sasa na unakuja baada ya tetesi zilizozagaa mwishoni mwa mwaka 2012 na mwanzoni mwa mwaka 2013 kwamba Facebook na Google walikuwa wakipigana vikumbo kutaka kuimiliki huduma hiyo maarufu ya utumaji ujumbe.


"WhatsApp inaelekea kuwaunganisha watu bilioni 1. Huduma inayofikia kiwango hicho ni huduma yenye thamani kubwa,” amesema mwanzilishi wa Facebook, Mark Zuckerberg, katika taarifa yake. "Ninamjua Jan [Koum, mwanzilishi wa WhatsApp] kwa muda mrefu na nimefurahi sana kushirikiana naye pamoja na timu yake ili kuzidi kuifungua na kuiunganisha dunia.”
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment