AJALI YA NDEGE YAUA 11 TUNISIA

Ndege ya jeshi la Libya iliyoanguka leo nchini Tunisia na kuua watu wote waliokuwemo.


Kwa uchache watu 11 wamepoteza maisha baada ya ndege moja ya madaktari wa jeshi la Libya kuanguka kusini mwa mji mkuu wa Tunisia, Tunis,  baada ya injini kushindwa kufanya kazi.

Kwa mujibu wa msemaji wa huduma za dharura wa Tunisia, bwana Mongi El Kadhi, ndege hiyo ilikuwa na watu 11 ambapo watatu walikuwa madaktari, wagonjwa wawili na wafanyakazi sita.

Ndege hiyo iliteketea kabisa na hakuna aliyenusurika katika ajali hiyo.

Muda mfupi kabla ya ndege hiyo kutoweka katika udhibiti wa rada, rubani aliwasiliana na uwanja wa ndege wa Tunis na kuwaambia kuwa injini ilikuwa imeshindwa kufanya kazi.


Ndege hiyo iliangukia shambani katika kijiji cha Nianou lakini iliweza kuzikwepa nyumba zote.


Huku uchunguzi ukiendelea kubaini chanzo cha ajali hiyo, inaelezwa kuwa hiyo ni ndege ya pili ya kijeshi kuanguka ndani ya wiki mbili katika eneo la Kaskazini mwa Afrika.
Mapema Februari 11 ndege ya jeshi la Algeria ilianguka milimani kutokana na hali mbaya ya hewa na kuua watu 77 ikiwa ni ajali mbaya kabisa ya ndege kuikumba nchi hiyo ndani ya muongo mmoja.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment