WATU KADHAA WAUAWA KATIKA MAPIGANO YA KIKABILA NCHINI KENYA

Security forces walk in Kainuk, in northern Kenya, on November 24, 2013 during a rescue operation.
Askari wa Kenya katika eneo la Kainuk, kaskazini mwa nchi hiyo, Novemba 24, 2013 katika mojawapo ya operesheni za uokozi.




Ripoti kutoka kaskazini mwa Kenya zinasema kuwa watu kadhaa wameuawa katika wiki ya mapambano kati ya makundi hasimu ya kikabila.

Kwa mujibu wa ripoti kutoka eneo hilo, kwa uchache watu 27 wameshapoteza maisha na zaidi ya 32,000 kukosa makazi kwa zaidi ya wiki moja sasa.

Gazeti la Kenya, la Standard Digital, limeripoti kuwa mapambano makali yalikuwa yakiendelea katika mji wa mpakani wa Moyale. Familia nyingi zimelazimika kukimbilia nchini Ethiopia.

Shirika la Msalaba Mwekundu nchini humo limesema kuwa jamii zilizokosa makazi zinatoka katika maeneo ya Butiye, Arosa na Gurumesa mjini Moyale.

"Watu kadhaa wameyakimbia makazi yao tangu Jumanne wiki hii baada ya mapigano kuongezeka. Baadhi walilazimika kukimbilia kwa ndugu zao katika miji ya Wajir na Marsabit. Watu hawa wanahitaji msaada wa chakula, makazi, maji, vyombo vya kupikia, nguo na vyandarua,” alisema mratibu wa shirika hilo katika mji wa Moyale Stephen Bonaya.

Serikali ya Kenya imeagiza kupelekwa kwa wanajeshi katika eneo hilo, huku wakazi wakiamini kuwa polisi walitoa mwanya watu hao wenye silaha wa kupigana mpaka walipoishiwa risasi ndipo wakaja.


Nchini Kenya kumekuwepo na mapigano mengi ya kikabili ambayo husababishwa na kugombania maji na malisho, jambo linalosababisha kuwepo kwa mashambulizi ya mara kwa mara ya kulipiza kisasi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment