WATU 300 WAMEUAWA AFRIKA YA KATI

Seleka soldiers sit in a pick-up truck in Bangui, the Central African Republic, on December 6, 2013.
Askari wa Seleka




Shirika la Msalaba Mwekundu limesema kuwa kwa uchache watu 300 wameuawa katika ghasia zinazoendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati tangu alhamisi.

Shirika hilo la kimataifa la misaada ya kiutu limesema kuwa limekusanya miili 281 ya watu waliouawa wakati wa siku mbili za ghasia katika mji mkuu wa nchi hiyo, Bangui.

Kiongozi wa Shirika hilo, Antoine Mbao Bogo, ameonya kuwa idadi ya vifo natarajiwa kuongezeka wakati wafanyakazi wa shirika hilo watakapoendelea na kazi ya kukusanya miili leo Jumamosi.

Wakati hali ikiwa hivyo, juzi Alhamisi, Ufaransa ilitangaza kuwa itatuma askari nchini humo.

Rais Francois Hollande alitoa tangazo hilo muda mfupi baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupitisha azimio la kutuma vikosi kwenda kudhibiti hali nchini humo.

Baraza hilo lenye wanachama 15 lilipitisha kwa kauli moja azimio linalovipa vikosi ya Umoja wa Afrika na vile vya Ufaransa idhini ya kwenda nchini humo. Kwa mujibu wa azimio hilo, askari wapatao 3,600 wa Umoja wa Afrika na 1,200 wa Ufaransa wameruhusiwa kwenda kudhibiti ghasia zinazoendelea kupoteza maisha ya watu.  

Hollande aliahidi kuwa askari 600 wa Ufaransa ambao tayari wapo Jamhuri ya Afrika ya Kati wataongezwa mara dufu ndani ya siku kadhaa au hata saa kadhaa, akisema kuwa nchi hiyo imeiomba Ufaransa msaada wa kuingilia kati naye ameamua kuitikia ombi hilo bila kuchelewa.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, Nicolas Tiangaye, ambaye alikuwa  Paris katika kilele cha Mkutano wa Ufaransa na Mataifa ya Afrika, aliitaka Ufaransa kuchukua hatua za haraka.

“Kutokana na dharura, ninatamani uingiliaji kati ufanyike mapema iwezekanavyo, mara tu baada ya azimio,” alisema Tiangaye.

Mnamo Novemba 21, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Laurent Fabius aliielezea Jamhuri ya Afrika ya Kati kuwa ni nchi iliyo katika ukingo wa kuangukia katika mauaji ya kimbari, akisema kuwa Ufaransa, majirani wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na jumuiya ya kimataifa wana wasiwasi juu ya machafuko nchini humo.

Jamhuri ya Afrika ya Kati iliingia katika machafuko baada ya muungano wa waasi ujulikanao kama Seleka, kuanzisha mashambulizi dhidi ya rekali mwezi Desemba 2012 na hatimaye mwezi Machi wakafanikiwa kumng’oa madarakani aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Francois BozizĂ©. Waasi hao wamekuwa wakishutumiwa kwa mauaji, unyang’anyi na ubakaji nchini humo.

Septemba 13, rais wa nchi hiyo, Michel Djotodia, aliuvunja muungano wa Seleka uliomuingiza madarakani. Baadhi ya waasi waliingia katika jeshi rasmi la serikali huku wengine wakiachwa.

Ripoti ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa inawashutumu waasi wa Seleka kwa ghasia nchini humo, ikisema kuwa waasi hao pamoja na makundi mengine yenye silaha wafanya vitendo vya ubakaji, unyang’anyo, udhalilishaji wa wanawake na watoto, kufanya mauaji, kutoa mafunzo ya kijeshi kwa watoto na kufanya mashambulizi na hujuma mbalimbali.


Mwezi Julai, Shirikisho la Kimataifa la Haki za Binadamu lilisema kuwa tokea  mwezi Machi kwa uchache mauaji 400 yanayohusishwa na kikundi cha Seleka yalikuwa yamesajiliwa.


Jamhuri ya Afrika ya Kati ina utajiri mkubwa wa rasilimali za madini kama vile dhahabu na almasi. Hata hivyo, nchi hiyo imekuwa ikikabiliwa na mfululizo wa matukio ya uasi na mapindzui tangu ilipojipatia uhuru wake mwaka 1960 kutoka kwa Ufaransa.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment