NYOTA WA MUVI YA ‘FAST AND FURIOUS' AFARIKI DUNIA


‘Fast and Furious' actor Walker dies in car crash


NYOTA maarufu wa muvi za “Fast and the Furious”, amefariki katika ajali ya gari Kusini mwa California.

Kwa mujibu wa ujumbe kutoka kwenye akaunti yake ya Twitter, Walker, aliyekuwa na umri wa miaka 40, ambaye ameonekana katika sehemu tano kati ya sita za filamu hizo zinazohusu matendo ya kihalifu mtaani, alipata ajali wakati akisafiri katika gari ya rafiki yake na alikuwa akielekea kwenye tukio moja la hisani.

“Kwa masikitiko makubwa, ninathibitisha kuwa Paul amefariki dunia mchana wa leo katika ajali ya gari,” msemaji wa Walker, Ame Van Iden, alisema katika barua pepe.

Polisi ya mji wa Los Angeles imetoa taarifa ikisema kuwa watu wawili walikufa katika ajali ya gari katika eneo la Valencia, na walipofika katika eneo la tukio walikuta gari ikiwa imezungukwa na moto. Ilitangazwa kuwa wahusika walifariki dunia hapo hapo.

Katika movi hiyo ya “Fast and Furious” yenye mfululizo kadhaa, nyota huyo amecheza kama Brian O'Conner akiwa kama afisa wa polisi.

Kampuni ya Universal imesema katika taarifa kuwa sehemu ya kwanza ya muvi hiyo, ilitolewa mwaka 2001, na mauti yamemkuta huku sehemu ya saba ikiwa inaendelea.


Kwa mojibu wa tovuti ya IMDb.com, Paul William Walker IV alizaliwa mjini Glendale, California, mwaka 1973 na kuanza kucheza filamu katika umri mdogo sana na kuonekana katika matangazo mbalimbali ya biashara.

Katika muvi ya “Monster in the Closet” ilitoka mwaka 1987 alicheza kama Professor Bennet na kuigiza kama nyota katika muvi ya “Throb”.

Alishiriki katika vipindi mbalimbali maarufu vya televisheni na kuonekana katika filamu mbalimbali kama vile “Timeline,” “Into the Blue,” “The Lazarus Project”,  “Hours,” ambayo itatoka mwezi huu wa Desemba na nyingine nyingi.


Kwa mujibu wa tovuti hiyo ya IMDb, Walker ameacha mtoto mmoja wa kike aitwaye  Meadow.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment