MIILI YA ASKARI WA ZAMANI YAGUNDULIKA KATIKA KABURI LA PAMOJA

Malian military junta leader Amadou Sanogo (C) arriving at the airport in Bamako.(File photo)
kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi nchini Mali, Amadou Sanogo –katikati- akiwasili katika uwanja wa ndege wa Bamako


Miili 21 imepatikana katika kaburi la pamoja katika mji wa Diago karibu na mji mkuu wa Mali, Bamako, kufuatia kukamatwa kwa kiongozi wa mapinduzi ya kijeshi ya mwaka jana.

Miili hiyo inayoaminika kuwa ya askari watiifu kwa rais aliyeondolewa madarakani, Amadou Toumani Touré, imepatikana usiku wa kuamkia leo.

Afisa mmoja wa usalama nchini humo amethibitisha taarifa hizo na kusema kuwa vitambulisho vilivyopatikana katika kaburi hilo vinaonesha kuwa ni kikosi maalumu cha askari wa jeshi la nchi hiyo.

 Tukio hilo limetokea wiki moja baada ya kiongozi wa mapinduzi ya mwaka 2012 dhidi ya rais Touré, Amadou Haya Sanogo, pamoja na watu wengine kumi na tano, wengi wakiwa askari na wapambe wake, kukamatwa hivi karibuni.

Rais wa zamani wa nchi hiyo, Amadou Toumani Touré, aliondolewa madarakani katika mapinduzi ya kijeshi yaliyofanyika Machi 22, 2012, na kuitumbukiza nchi hiyo ya Afrika Magharibi katika mzozo uliolifanya kundi la waasi wa Kituareg lenye mafungamano na al-Qaeda kulidhibiti eneo lote la upande wa kasikazini mwa nchi hiyo.

Kwa mujibu wa serikali ya Mali, Sanogo ameshitakiwa kwa makosa ya kuteka na kuua.

Kufuatia kuongezeka kwa uasi nchi humo, mwezi Januari Ufaransa iliamua kuingilia kati kijeshi katika koloni lake hilo la zamani ikionesha wasiwasi dhidi ya kuongezeka kwa ushawishi na nguvu za wapiganaji kaskazini mwa nchi hiyo na kuongezeka kwa uasi wa Kituareg wanaotaka kujitenga kwa eneo hilo kiasi cha kutishia kuanguka kwa serikali.


Mwezi Februari, shirika la Amnesty International lilielezea kuwepo kwa ukiukwaji wa haki za binadamu nchini humo, ikiwa ni pamoja na kuuawa kwa watoto.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment