HIZBULLAH YAPATA PIGO


·        



Vuguvugu la Hizbullah la nchini Lebanon limesema kuwa mmoja wa makamanda wake, Hassan al-Laqqis ameuawa asubuhi ya leo nyumbani kwake karibu na mji mkuu wa nchi hiyo, Beirut.

Katika taarifa yake iliyosomwa leo katika kituo cha televisheni cha al-Manar cha nchini humo, kundi hilo limesema kuwa kamanda huyo aliuawa katika mji wa Hadath yalipokuwa makazi yake, limeilaumu Israeli kuwa ndiyo iliyotekeleza mauaji hayo.

"Lawama za moja kwa moja tunaelekezwa kwa adui yetu Israeli ambayo kwa muda mrefu ilikuwa ikijaribu kumuua ndugu yetu na katika maeneo mbalimbali lakini mara zote ilishindwa, mpaka jana jioni,” ilisema taarifa hiyo ya Hizbullah.

"Adui huyu lazima abebe dhima na matokeo ya jinai hii ya kinyama,” iliongeza taarifa hiyo.

Mpaka sasa Israeli haijatoa kauli yoyote kuhusu madai na tuhuma hizo zilizoelekezwa kwake kutoka upande wa Hizbullah.

Hata hivyo, kundi moja nchini Lebanon limeelezea kuwa limehusika na mauaji hayo.

Itakumbukwa kuwa utawala wa Israeli uliishambulia Lebanon katika vita mbili za mwaka 2000 na 2006. Watu wapatao 1,200, wengi wao wakiwa raia wa kawaida, waliuawa katika vita ya mwaka 2006 iliyodumu kwa muda wa siku 33.

Hata hivyo, katika matukio yote mawili vikosi vya Israeli vilishindwa kutimiza malengo yake na kurejea nyuma.


Mwezi Agosti 2012, katibu mkuu wa Hizbullah, Seyyed Hassan Nasrallah, alisema kuwa kundi lake lina uwezo na ujasiri wa kuitetea Lebanon na kwamba makombora yake yapo tayari kujibu shambulizi lolote litakalofanywa na Israeli dhidi ya Lebanon.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment