BUNGE LA SOMALIA LAMNG’OA WAZIRI MKUU

File photo of Somali Premier Abdi Farah Shirdon
Waziri Mkuu wa Somalia Abdi Farah Shirdon




Bunge nchini Somalia limepitisha kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Abdi Farah Shirdon, kufuatia miezi kdhaa ya mgogoro baina ya waziri mkuu na rais wa nchi hiyo.

Jumla ya wabunge 184 kati ya 250 waliohudhuria walipiga kura ya kumuondoa wakiilaumu serikali yake iliyoingia madarakani mwaka mmoja uliopita kuwa ni dhaifu.

Waziri Mkuu huyo amekuwa na mgogoro na Rais Hassan Sheikh Mohamoud kuhusu kuundwa kwa baraza jipya la mawaziri, jambo lililosababisha kupigwa kwa kura hiyo ya kutokuwa na imani naye.

Wabunge wanalituhumu baraza la mawaziri kuwa limeshindwa kuongoza nchi na kwamba serikali iliyong’olewa ilikuwa dhaifu.

Kabla ya kura hiyo, waziri mkuu alisema kuwa mgogoro baina yake na rais ulikuwa wa kikatiba na ulihitajika kuamuliwa na wabunge.

Hata hivyo, rais alisema kuwa hakutaka Waziri Mkuu huyo ajiuzulu licha ya mkwamo huo wa kisiasa uliodumu kwa miezi kadhaa.

Wataalamu wanasema kuwa itachukua miezi kadhaa kabla ya kuteuliwa kwa baraza jipya la mawaziri na kisha kupitishwa na bunge.


Somalia imekuwa bila serikali kuu yenye nguvu tangu mwaka 1991, baada ya wababe wa vita kumuondosha aliyekuwa rais wa wakati huo, Mohamed Siad Barre.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment