WAANDAMANAJI WACHOMA MOTO OFISI ZA CHAMA TAWALA



File photo of Tunisians shouting slogans in a protest rally outside Interior Ministry in Tunis, on February 6, 2013.
Waandamanaji nchini Tunisia

Waandamanaji nchini Tunisia wamezichoma moto ofisi za chama tawala cha Annahda katika mji wa Qafsa, katikati mwa nchi hiyo.

Waandamanaji hao walizichoma ofisi hizo baada ya kujaribu kuingia katika ofisi za mkuu wa mkoa huo.

Polisi walifanikiwa kuwafukuza, lakini tayari walikuwa wameshachukua makabrasha na samani za ofisi na kuzichoma moto barabarani.

Tukio hilo lilifuatia maandamano makubwa katika mji hu ona miji mingine kama Gabes na Siliana, ambayo yaliitishwa kupinga umasikini na ukosefu wa maendeleo.

Novemba 15, waandamanaji walikusanyika katika mji mkuu wa nchi hiyo wakitaka chama tawala kiondoke madarakani.

Baada ya miezi kadhaa ya mgogoro wa kisiasa, chama tawala na upinzani walianzisha mazungumzo Oktoba 25 ili kuunda serikali ya mpito inayoundwa na watu huru wasiogemea upande wowote ambayo ingeiongoza nchi hiyo mpaka uchaguzi ujao.

Tunisia imekuwa katika mgogoro tangu mapinduzi ya mwaka 2011 yaliyomng’oa madarakani rais wa zamani wa nchi hiyo, Zainul Abideen bin Ali/

Hali hiyo ilizidi kuwa mbaya baada ya watu wenye silaha kuwa kumuua kiongozi maarufu wa upinzani, Muhammad Brahmi, mwezi Julai baada ya kiongozi mwenzake Chokri Belaid, kuuawa mwezi Februari.


Hali mbaya ya kiuchumi, kama ilivyo katika nchi nyingi za Kiafrika, ni miongoni mwa vichocheo vya ghasia hizo, ambapo mfumko wa bei unakadiriwa kufikia asilimia 6 na nakisi ya bajeti ni asilimia 7.4 ya mapato ya ndani.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment