SHERIA MPYA YA MAANDAMANO YAZIDI KUPANDISHA JOTO LA KISIASA NCHINI MISRI



Egyptian activists shout slogans against the Egyptian military in Cairo, November 27, 2013.
Waandamanaji wakipaza sauti kupinga utawala wa kijeshi mjini Cairo Novemba 27, 2013


Na Kabuga Kanyegeri, Istanbul


Joto la kisiasa nchini Misri limeendelea kuwa juu baada ya mahakama moja kuwapa adhabu ya kifungo cha miaka 11 jela mabinti 21, huku maimam 17 wa misikiti wakikamatwa katika mji wa Gharbeya kwa kile kinachodaiwa kuwa wamefanya uchochezi dhidi ya jeshi.

Kwa mujibu wa gazeti la al-Shorouk la nchini humo, mahakama hiyo ndogo katika mji wa Alexandria imewapa adhabu mabinti hao 21 kwa sababu ya kushiriki katika maandamano ya kuipinga serikali ya mpito iliyowekwa madarakani na jeshi la nchi hiyo.

Aidha, kwa mujibu wataarifa zilizotolewa na vyombo vinavyoliunga mkono Vuguvugu la Udugu wa Kiislamu (Muslim Brotherhood), wanafunzi kadhaa walikamatwa na polisi ya nchi hiyo baada ya kuingia katika makazi ya wanafunzi hao katika chuo kikuu cha al-Fayoum.

Polisi waliingia katika majengo cha hicho wakafyatua gesi ya kutoa machozi na kuwakamata wanafunzi kadhaa waliokuwa wakipanga kufanya maandamano dhidi ya mapinduzi yaliyofanywa na jeshi.

Katika ripoti nyingine, mwendesha mashitaka nchini humo ameagiza kuwaweka kizuizi kwa siku nne wanaharakati 24 waliokamatwa wakati wa maandamano ya kupinga sheria mpya inayowatia hatiani wale wanaoandamana bila kibali.

Adiha, kibali cha kikamatwa kimetolewa dhidi ya wanaharakati maarufu wanaotuhumiwa kuwachochea waandamanaji kufanya maandamano.

Mamlaka nchini humo zinamsaka mwanaharakati mashuhuri Alaa Abdul Fatta na Ahmad Maher, muasisi wa vuguvugu la Aprili 6 lililoongoza mapinduzi dhidi ya aliyekuwa rais wa zamani wa nchi hiyo, Husni Mubarak mwaka 2011.

Siku ya jana, vikosi vya usalama vilitumia maji ya kuwasha kuwatawanya watu waliokuwa wakiandamana nje ya bunge la seneti mjini Cairo.

Waandamanaji hao walikuwa wakipinga mabadiliko ya muswada wa katiba yatakayoruhusu raia kushitakiwa katika mahakama za kijeshi.

Mnamo Novemba 24, nchi hiyo ilianzisha sheria yenye utata ambayo mikusanyiko ya zaidi ya watu 10 itahitaji kibali siku tatu kabla ya kufanyika.


Operesheni ya vikosi vya usalama vya nchi hiyo dhidi ya waandamanaji imekuwa ikikoselewa vikali na Kamishna wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Navi Pillay, na shirika la kimataifa la haki za binadamu, Amnesty International.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment