VOLKANO YAWAHAMISHA WATU 5,000

Indonesia
Mlima Merapi, Indonesia




Na Kabuga Kanyegeri

MFULULIZO wa milipuko ya volkano imewahamisha watu wapatao 5,000 kutoka katika vijiji saba magharibi mwa Indonesia.

Watu wanaoishi umbali wa kilometa tatu (maili1.9) kutoka eneo la volkano wamehamishwa kutoka kwenye nyumba na makazi yao.

Kwa mujibu wa wakala wa kitaifa wa kushughulikia majanga nchini humo, Mlima  Sinabung ulioko kaskazini mwa kisiwa cha Sumatra umekuwa ukitema majivu mekundu yenye joto, mawe na lava nyingi na nzito na kuirusha juu umbali wa kilometa 7 (4 maili) tangu mwanzoni mwa mwezi huu wa Novemba.

Indonesia ni eneo lenye wingi wa volkano hai na ipo katika ukanda unaojulikana kama “Ulingo wa Moto” (Ring of Fire) uliopo baina ya Bahari ya Pacific na Bahari ya Hindi.


Mwaka 2010, zaidi ya watu 350 walipoteza maisha yao kufuatia mfululizo wa milipuko ya volkano katika Mlima Merapi katikati mwa eneo la Java.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment