MAFURIKO YAUA 300 KASKAZINI MASHARIKI MWA SOMALIA


Picture released on November 12, 2013 by the African Union information services shows an aerial view of flooding in and around Jowhar town on November 12, 2013.
Picha iliyotolewa Novemba 12, 2013 na Kituo cha Habari cha Umoja wa Afrika ikionesha hali ya mafuriko katika mji wa Jowhar. 



WATU wapatao 300 wanahofiwa kupoteza maisha katika jimbo la Putland, kaskazini mashariki mwa Somalia, kufuatia tufani kali na mafuriko makubwa yaliyolirikisa jimbo hilo.

Kwa mujibu wa taarifa ya serikali iliyotolewa leo, mvua kubwa, upepo mkali na mafuriko vimesababisha hali ya hatari, ambapo watu 300 wanahofiwa kupoteza maisha, mamia wengine hawajulikani walipo, mifugo mingi imepotea, vijiji, makazi na majengo vimeharibiwa vibaya.

İdadi hiyo ya vifo haijathibitishwa na duru huru; hata hivyo, wataalamu wa masuala ya hali ya hewa kutoka Shirika la Kimataifa linaloshughulika na Chakula na Kilimo (FAO) wamesema kuwa mafuriko hayo nim abaya sana.

"Puntland ni jimbo kavu, na mvua hainyeshi sana, lakini ikinyesha kwa kiwango tunachokiona sasa, athari yake huwa mbaya sana,” alisema Hussein Gadain, mshauri wa ufundi kutoka FAO.

Shirika la Chakula Duniani (WFP) limesema kuwa linafanya kazi na maafisa wa jimbo hilo kutathmini mahitaji ili kujaribu kuwahudumia watu walioathiriwa na tufani hiyo iliyoanza siku ya Jumamosi.

Barabara inayounganisha mji mkuu wa jimbo la Puntland, Garowe na mji wa bandari wa Bossaso imekatika na hivyo kukwamisha shughuli za upelekaji misaada.

Puntland ni ngome ya maharamia wanazishambulia meli zinazopita kwenye pwani ya jimbo hilo. İngawa jimbo hilo lina utajiri wa nishati, lakini wakazi wake ni masikini. 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment