UFILIPINO YAZIDI KUANDAMWA NA MABALAA



WAKIWA bado katika maumivu ya kukumbwa na gharika kubwa iliyosababishwa na kimbunga Haiyan kilichosababisha vifo vya maelfu, Ufilipino imekumbwa na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 4.8 katika kisiwa cha Bohol.

Kitovu cha tetemeko hilo kilikuwa katika mji wa San Isidro, kilometa 45 kutoka mji mkubwa wa kisiwa hicho, wa Tagbilaran, wenye wakazi 100,000.
Taarifa kutoka Taasisi ya Volkanolojia na Seismolojia ya nchi hiyo imesema kuwa tetemeko hilo lilipiga kilometa 70 kutoka chini ya ardhi.

Hakuna maafa yaliyoripotiwa na mamlaka hazijatoa tahadhari ya tsunami kufuatia tetemeko hilo.

Mwezi uliopita, tetemeko liliua watu 22 na wengine maelfu kukosa makazi. Vilevile lilisababisha uharibifu wa zaidi ya nyumba 73,000.

Kisiwa cha Bohol kipo kusini mwa eneo lililopitiwa na kimbunga kikali cha Haiyan, ambacho nchini humo kinajulikana kama Kimbunga Yolanda.

Kimbunga hicho, ambacho ndio kikubwa zaidi kuikumba nchi hiyo kwa miongo kadhaa, kilisababisha vifo vya zaidi ya watu 20,000 na kubomoa maelfu ya nyumba. Serikali ya nchi hiyo imetengaza hali ya janga la kitaifa huku juhudi za uokozi zikiendelea.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment