MKATABA WA AMANI YA KONGO WAKWAMA

Congolese M23 rebels gather inside an enclosure after surrendering to Uganda
Wapiganaji wa M23 wamekusanyika ndani ya uzio baada ya kujisalimisha kwa serikali ya Uganda katika kijiji cha Rugwerero, takriban kilometa 500 magharibi mwa mji mkuu wa Uganda, Kampala.




Na Kabuga Kanyegeri

MKATABA wa amani uliokuwa ukitarajiwa kusainiwa baina ya serikali ya Kongo na waasi wa M23 umeakhirishwa baada ya maafisa wa serikali kuomba muda zaidi wa kuupitia mkataba hu.

Msemaji wa serikali ya Uganda, Ofwono Opondo, amesema jana kuwa muafaka utalazimika kusubiri mpaka serikali ya Kongo itakapofikia uamuzi wake.

Mkataba huo ambao ulitarajiwa kusainiwa jana katika mji wa Entebbe nchini Uganda, ni hatua muhimu ya kumaliza miongo kadhaa ya vita nchini humo.

Naye Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Uganda, Okello Oryem, alisema kuwa makubaliano hayakufikiwa baada ya serikali ya Kongo kusisitiza kuwa itasaini “azimio” la kwamba uasi umekwisha badala ya kufanya “makubaliano” na waasi walioshindwa vita, suala linaloonesha ugumu katika kuzisuluhisha pande mbili.

Maafisa wa Kongo hawakutoa maelezo yoyote kuhusu hali hiyo na haijatangazwa tarehe ya kikao kingine baina ya pande hizo.

Hivi karibuni mamia ya waasi wa M23 walikimbilia Uganda baada ya kushindwa na vikosi vya jeshi la Kongo, ambalo linasaidiwa na brigedi maalumu ya Umoja wa Mataifa inayoongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania.

Mnamo Novemba 5, kundi la M23 lilisema kuwa litaweka silaha chini na kuingia katika mazungumzo ya amani baada ya ngome zake za milimani katika vijiji vya Tshanzu na Runyoni kwenye mpaka wa Uganda na Rwanda kudhibitiwa na vikosi vya serikali ya Kongo.

Makundi kadhaa yenye silaha, ikiwemo M23, wanaendesha harakati zao za uasi mashariki mwa Kongo na wanapigania kuidhibiti nchi hiyo kubwa yenye maliasili za madini, kama vile dhahabu, urani, coltan, ambayo hutumika katika utengenezaji wa vifaa vingi vya elektroniki, ikiwemo simu za mkononi.

Waasi wa M23 waliuteka mji wa Goma Novemba 20, 2012 baada ya walinda amani kuondoka  katika mji huo wenye wakazi milioni moja. Wapiganaji wa M23 waliondoka katika mji huo Desemba 1,2013 baada ya makubaliano ya kusimamisha mapigano.

Waasi wa M23 walijiondoa katika jeshi la Kongo mwezi Aprili 2012 kupinga kile walichodai kuwa ni mwenendo mbaya ndani ya jeshi la Taifa (FARDC). Walikuwa wamejumuishwa katika jeshi chini ya mkataba wa amani uliosainiwa mwaka 2009.

Tangu mwezi Mei 2012, takriban watu milioni 3 wameyekimbia makazi yao katika eneo la mashariki mwa Kongo. Takriban watu milioni 2.5 ni wakimbizi wa ndani, huku zaidi ya watu 460,000 wamekimbilia katika nchi za Rwanda na Uganda.


Kongo imekuwa ikikabiliwa na matatizo matatizo kwa miongo kadhaa, kama vile umaskini uliokithiri, miondombinu mibovu, na vita katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo ambavyo viliibuka tangu mwaka 1998 na kugharimu maisha ya zaidi ya watu milioni 5.5.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment