CHAMA TAWALA NIGERIA KATIKA MGAWANYIKO MKUBWA

File photo of Nigerian President Goodluck Jonathan
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan





Magavana 7 katika majimbo saba yenye nguvu nchini Nigeria wamejiunga katika muungano mpya wa upinzani na hivyo kumpa wakati mgumu Rais Goodluck Jonathan katika mbio zake za kutaka kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Chama kikuu cha upinzani nchini humo cha All Progressives Congress (APC), kimetangaza kuwa magavana wa majimbo saba wamejiunga na chama hicho, ingawa kuna ripoti zinazoashiria kuwa magavana wawili au watatu bado hawajaamua kujiunga na upinzani.

Wakati huohuo, chama cha Rais Jonathan cha Peoples Democratic Party (PDP) kimesema kuwa hatua ya magavana hao ni hatua chanya kwa sababu imeondosha hali ya mvurugano ambayo ingetokea ndani ya chama.

Mwezi Septemba, Rais Jonathan aliwatimua mawaziri tisa kutokana na mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hicho tawala.

Magavana hao saba pamoja na mgombea wa zamani wa kiti cha urais, Atiku Abubakar, aliyejiondoa katika chama cha Rais Jonathan Agosti mwaka huu, wameunda mmungano wa upinzani ili kumuwezesha kugombea tena katika uchaguzi ujao wa mwaka 2015.

Kwa sasa chama hicho cha upinzani cha APC kinadhibiti majimbo 17 yenye wapiga kura milioni 33 waliojiandikisha, huku chama tawala cha PDP kikidhibiti majimbo 15 tu yenye wapiga kura milioni 26 waliojiandikisha.


Rais Jonathan alichaguliwa tena mwaka 2011, kufuatia kifo cha aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Umar Yar Adua mwaka 2010.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment