KIONGOZI WA MTANDAO WA HAQQANI AUAWA



KIONGOZI mwandamizi wa kundi la wapiganaji wa mtandao wa Haqqani, nchini Pakistan, wenye mafungamano na Talibani amepigwa risasi na kuuawa.

Maafisa upelelezi wa Pakistan wanasema kuwa Nasiruddin Haqqani, ndugu wa  Sirajuddin Haqqani, ameuawa jirani na mji wa Islamabad mwishoni mwa juma.

Duru zinasema kuwa mwili wake ulipelekwa katika mji wa Miranshah, mji mkubwa katika jimbo la Kasikazini la Waziristan kwa ajili ya mazishi.

Mauaji ya kiongozi huyo yanakuja siku kadhaa baada ya shambulizi la ndege za Marekani zisizokuwa na rubani (drone) kumuua kiongozi wa kundi la Taliban nchini Pakistan, Hakimullah Mehsud, pamoja na watu wengine wanne katika eneo la kaskazini magharibi mwa Pakistan lenye hali mbaya kiusalama.


Mtandao wa wapiganaji wa Haqqani, wenye mafungamano na wapiganaji wa al-Qaeda, umekuwa ukifanya mashambulizi makali ndani ya Pakistan na katika nchi jirani ya Afghanistan.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment