HALI YA KIBINADAMU UKANDA WA GAZA INAZIDI KUWA TETE

A Palestinian woman and her children light candles during a power outage in Gaza City on November 10, 2013.
Mwanamke wa Kipalestina na wanaye wakiwasha mishumaa baada ya ukame wa umeme kulikumba eneo la Gaza Novemba 10, 2013.




Na Kabuga Kanyegeri


ENEO la Ukanda wa Gaza linakabiliwa na hali mbaya ya kibinadamu ambapo Wapalestina wanaoishi katika eneo hilo la pwani wameendelea kukosa umeme kutokana na mzingiro wa miaka 6 ulioweka na utawala wa Israeli katika eneo hilo.

Mzingiro huo unawafanya wakazi hao kutokuwa na uwezo wa kuingiza bidhaa na huduma mbalimbali.

Hali ya kibinadamu imezidi kuwa mbaya kutokana na kinu pekee cha kufua umeme kusitisha shughuli zake tangu Novemba 1 kutokana na ukosefu wa mafuta.

Katika miezi ya hivi karibuni, upungufu wa mafuta na umeme umekithiri na kushtadi baada ya jeshi la Misri kuziba na kuzifunga njia za chini kwa chini zilizokuwa zikisaidia kupeleka bidhaa na huduma katika eneo hilo. Njia hizo zilikuwa zikisaidia kuokoa maisha ya wakazi wa Gaza wapatao milioni 1.7.

Wakati huo huo, maafisa katika eneo la Gaza wanasema kuwa baadhi ya wakazi hao wameanza kutumia maji machafu kutokana na mashine ya usafishaji wa maji kuacha kufanya kazi kutokana na ukame wa nishati.

Kinu hicho cha kusafisha maji kilikuwa kikiwahudumia wakazi 120,000. Maafisa hao wanasema kuwa mashine nyingine zitaacha kufanya kazi hivi karibuni kutokana na ukosefu wa nishati. Manispaa ya mji wa Gaza imetangaza hali ya dharura, na wataalamu wameonya kutokea kwa janga la kimazingira.

Ukanda wa Gaza umekuwa katika mzingiro tangu mwaka 2007, hali ambayo imewafanya Wapalestina hao kutegemea bidhaa na huduma kuwafikia kupitia njia za chini kwa chini ambazo zimefungwa na watala wa sasa wa Misri.

Mtandao wa mashirika na taasisi za Kipalestina (PNGO), ambao unawakilisha zaidi ya taasisi 130 za kiraia, umetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kukomesha mzingiro huo unaondelea kufanywa na utawala wa Israeli.

Mashirika kadhaa ya kiraia na ya haki za kibinadamu yamelikosoa jeshi la Misri kwa kuwanyima wakazi wa Gaza nafasi ya kupata huduma nyingi za msingi kama vile vifaa vya ujenzi, chakula na nishati.

Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment