POLISI WA ETHIOPIA WAYATAWANYA MAANDAMANO YA WANAOPINGA MAUAJI YA WENZAO WALIOUAWA SAUDIA

Ethiopians hold anti-Saudi rallies in Addis Ababa.
Waethiopia wakiandamana mjini Addis Ababa kupinga mauaji ya wenzao waliouawa nchini Saudia Arabia



POLISI nchini Ethiopia wametumia nguvu kutawanya mamia ya wananchi wa nchi hiyo waliokuwa wakiandamana kupinga mashambulzi yanayowalenga wafanya kazi wa Kiethiopia nchini Saudi Arabia.

Hayo yanakuja baada ya Waethiopia kukusanyika nje ya Balozi wa Saudia mjini Addis Abba kupinga kamata kamata inayofanywa na utawala wa Riyadh dhidi ya wahamiaji haramu.

Maandamano hayo yaliitishwa na Chama cha upinzani cha Vuguvugu la Bluu baada ya Waethiopia watatu kuua nchini Saudi Arabia. Waandamanaji walitoa wito wa kususia na kuzifunga biashara za Wasaudia nchini mwao. Wanaharakati wanasema kuwa polisi walifanya haraka sana kuyasambaratisha maandamano hayo.

Kwa mujibu wa afisa mwandamizi wa chama hicho, Getaneh Balcha, zaidi ya waandamanaji mia moja, wakiwemo mwenyekiti wa chama hicho cha upinzani na makamu wake wamekamatwa.

"Polisi walikuja na kutupiga, na sasa zaidi ya watu 100 wameshikiliwa katika kituo cha polisi,” alinukuliwa afisa huyo wakati akiongea na vyombo vya habari.

Wiki iliyopita, serikali ya Ethiopia ilithibitisha kuwa raia wake watatu waliuawa katika makabiliano na polisi wa Saudia.


Vifo vyao vilitokana na kamata kamata inayoendelea kufanywa na utawala wa Riyadh dhidi ya wahamiaji haramu wapatao elfu 23 wa Ethiopia pamoja na raia wengine wa kigeni. Waethiopia wengi husafiri kwenda Mashariki ya kati kila mwaka kutafuta kazi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment